• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

VIONGOZI WA USHIRIKA WATAKIWA KULIPA MADENI

Posted on: June 21st, 2022

                                             

Viongozi na wanachama wa vyama vya ushirika Mkoani Morogoro wameaswa kuondokana na tabia ya kutolipa madeni ya mikopo yao kwa wakati kwani kufanya hivyo kunapelekea kutostawisha vema mitaji ya vyama hivyo na kupelekea kuwa tegemezi.

Hayo yamebainishwa Juni 21 kupitia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela iliyosomwa kwa niaba yake na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga wakati wa kufunga maadhimisho ya Jukwaa la vyama vya ushirika Mkoani humo yaliyofanyika katika ukumbi wa Savoy katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga akizungumza na maafisa ushirika alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela wakati wa kufunga jukwaa la ushirika Mkoani humo Juni 21 mwaka huu.


Aidha, Mhe. Mstahiki Meya huyo amesema kuwa taasisi za mabenki pamoja na Sacoos za ushirika zinajiendesha kwa faida ambapo hutegemea mnyororo wa kukopa na kurudisha fedha kwa wakati hivyo kuchelewa kurejesha fedha hizo ni kukwamisha shughuli za taasisi na Saccos husika.

“Niwaagize viongozi na wanachama wote waliopo katika ukumbi huu kuhakikisha mnaacha tabia ya kutolipa madeni kwa wakati,hivyo ni kuchelewa kustawisha na kuongeza mitaji yenu” amesema Mhe. Mstahiki Meya.

Katika hatua nyingine Pascal Kihanga amewataka viongozi na mamlaka zinazosimamia vyama vya Ushirika Mkoani Morogoro kuongeza kasi ya kukagua na kusimamia kwa ukaribu na kuchukua hatua za haraka pindi inapoonekana Kuna taarifa za ukiukwaji wa sheria na miongozo ya vyama hivyo vya ushirika.



Kwa upande wake Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Morogoro Bw. Keneth Shemdoe amebainisha changamoto za kiutendaji za idara ya ushirika kama uhaba wa watumishi ngazi ya Mkoa na Halmashauri zake kuwa na idadi ndogo ya wanachama kulinganisha na idadi ya wakulima na baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika kutokuwa waaminifu hali inayopelekea kutokea kwa migogoro yaara kwa mara.


Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Morogoro Bw. Keneth Shemdoe akisoma taarifa ya ushirika wakati wa kufunga jukwaa la ushirika Juni 21 mwaka huu.



Aidha Bw. Shemdoe ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kuendelea kuchukua hatua na kutatua changamoto za ushirika hapa nchini kupitia ofisi ya mrajisi wa Mkoa kwa kuimarisha udhibiti wa misingi ya utawala bora na uwajibikaji wa vyama vya ushirika kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na kutatua migogoro kwa kutoa ushauri wa kisheria kwa vyama hivyo.





Akisoma risala kwa Mgeni rasmi, mwenyekiti wa Jukwaa la Maendeleo ya vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro Iddy Bilali pamoja na kueleza mafanikio yaliyopo katika jukwaa hilo, ameeleza changamoto wanazokumbana nazo zikiwemo za wanachama wa vyama vya ushirika kutorejesha mikopo kwa wakati, kukosekana kwa viwanda vya kusindika mazao pamoja wanunuzi kununua mazao ya wakulima kwa bei ndogo na kwenda kuyauza kwa bei ya juu hali inachangia kurudisha nyuma utendaji.


Mwenyekiti wa jukwaa la usirika Mkoa wa Morogoro Bw. Iddy Bilali akisoma risala ya jukwaa hilo mbele ya mgeni rasmi wakati wa kufunga kwa jukwaa hilo Juni 21 mwaka huu katika ukumbi wa Savoy Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Maafisa ushirika kutoka Halmashauri za Mkoa wa Morogoro wakiwa katika mkutano wa jukwaa la ushirika lililofanyika Juni 21 mwaka huu katika ukumbi wa Savoy Manispaa ya Morogoro.



Naye Bw. Philipo Mruto ambaye ni mwakilishi wa AMANI AMCOS na Mmiliki wa Mruto Solution ameshauri wakulima kushirikiana na vyama mbalimbali vya ushirika ili kuweza kupata masoko ya uhakika na bei zenye kuridhisha, kwani kuwa nje ya vyama hivyo ni kuruhusu utapeli na kuumiza wakulima kupitia bei ndogo za mazao.




Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga akiwa picha ya pamoja na baadhi ya maafisa ushirika wa Mkoa wa Morogoro (wa tatu kushoto ni Mrajisi wa Mkoa huo Bw. Keneth Shemdoe).



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.