• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

Posted on: May 1st, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka waajiri Mkoa wa Morogoro kuendelea kutatua changamoto za wafanya kazi wao ili kuleta chachu mahari pa kazi kwa maslahi mapana ya wafanyakazi wenyewe, wanamorogoro na Taifa kwa ujumla.


Wito huo umetolewa leo Mei 1, 2025 wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yenye kaulimbiu inayosema "Uchaguzi Mkuu 2025, Utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi, wafanyakazi tushiriki" Maadhimisho hayo yamefanyika uwanja wa Jamhuri uliopo Halmashauri  ya Manispaa ya Morogoro.


Mhe. Malima amesema kuna umuhimu wa waajiri kuwajali na kuwathamini wafanyakazi kwa kuwatatulia changamoto wanazokumbana nazo ili kuweza kuwapa motisha ya kufanya kazi kwa bidii na kuiletea kampuni husika maendeleo inayoyatarajia.


".. Nichukue fursa hii kuwaelekeza waajiri wote wa Sekta binafsi katika Mkoa wa Morogoro kutatua changamoto za wafanyakazi wao.." Amesisitiza Mhe. Adam Malima


Aidha, kiongozi huyo ameitaka Ofisi ya Afisa kazi Mkoa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye maeneo ya kazi ili kujiridhisha kama mikataba ya wafanya kazi inazingatia sheria za kazi na kubaini wanaovunja sheria.


Sambamba na hayo Mkuu huyo wa Mkoa amewataka viongozi wa OSHA Mkoani humo  kuhakikisha wanashughulikia malalamiko ya wafanya kazi na kuwachukulia hatua za kisheria waajiri wote wanaokiuka misingi ya kisheria na kukomesha baadhi ya tabia za baadhi ya waajiri kukiuka na kuwakandamiza wafanyakazi.


Kwa upande wa maslahi ya watumishi Mhe. Malima amesema Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha maslahi yao kwa kuwaongezea mishahara na kuendelea kutoa ajira na kupunguza changqmoto ya upungufu wa watumishi  ambapo mwaka 2023/2024 watumishi 741 waliajiriwa katika Halmashauri za Mkoa wa Morogoro na mwaka 2024/2025 jumla ya wafanya kazi 1491 wameajiriwa.


Kwa upande wa wafanyakazi kupitia risala iliyosomwa mbele ya mgeni rasmi, wameiomba Serikali kushughulikia changamoto zikiwemo madai mbalimbali ya wafanyakazi yakiwemo yanayohusu likizo, uhamisho, matibabu, kukaimu, kujikimu, stahiki za ajira mpya, malimbikizo ya mishahara kwa waliondolewa kazini kimakosa mwaka 2017 pamoja na malipo ya mafao ili kuhakikisha watumishi wanapata stahiki zao kwa mujibu wa sheria.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.