• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAALIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA USALAMA NA MALEZI BORA KWA WANAFUNZI.

Posted on: January 28th, 2023


Naibu Katubu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI Dkt. Charles Msonde akitoa hotuba ya kufunga mafunzo endelevu ya Walimu shuleni. 

Kutokana na ongezeko la vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto hapa nchini, maafisa elimu wameagizwa kusimamia kwa karibu usalama wa wanafunzi ndani na nje ya shule kwa lengo la kuwasaidia kutimiza ndoto zao.

Agizo hilo limetolewa Januari 28 mwaka huu na Dkt. Charles Msonde Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, kwenye hafla ya kuhitimisha Semina ya Mafunzo Endelevu ya Walimu shuleni (MEWAKA) iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo katika Chuo Cha Uwalimu Morogoro.

Dkt. Msonde amesema kuwa jambo la ukatili kwa watoto halikubaliki kutokana na uwepo wa matukio mengi ya ukatili na unyanyasaji hadi kwenye familia, jamii na shuleni hivyo walimu wanatakiwa kujiepusha na ukatili.

Aidha, Naibu Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa adhabu zitolewe kwa mujibu wa sheria hivyo wanatakiwa kuzingatia sheria hizo za utoaji wa adhabu kwa wanafunzi.

Washiriki wa mafunzo ya MEWAKA wakimsikiliza mgeni rasmi akitoa hotuba yake ya kuhitimisha mafunzo ya MEWAKA.

“... na jambo hili la ukatili halikubaliki kwa watoto, jambo hili linaonekana sio tu shuleni, linaonekana lipo kwenye jamii, linaonekana lipo nyumbani... tuzuie na kukataa ukatili wa watoto”. Amesema Dkt. Msonde.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Songwe ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Mkoani humo Bwana Michael Ligola amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuipa kipaumbele sekta ya elimu Kwa kuhakikisha sekta hiyo ina imarika.

Afisa Elimu Mkoa wa Songwe ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu  Bwana Michael Ligola akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi baada ya kuhitimishwa kwa Mafunzo Endelevu kwa Walimu kazini.

Aidha, Afisa Elimu huyo amemthibitishia mgeni rasmi kuwa lengo la mafunzo hayo ni kwenda kufanya mageuzi katika sekta ya elimu na kuhakikisha ujuzi walioupata unakuwa na matokeo.

Sambamba na hilo, Bw. Ligola kwa niaba ya walimu wenzake waliopata mafunzo ya MEWAKA kupitia semina hiyo ya siku mbili  amemuomba Naibu Katibu Mkuu huyo wa TAMISEMI kuwa na kikao cha tathmini ya mafunzo hayo ili kujua kama kile walichojifunza ndicho wanachokifanyia kazi katika maeneo yao pamoja  na kutatua kwa pamoja changamoto zitakazokuwa zimejitokeza kwa kipindi hicho kifupi.

Mgeni rasmi Dkt. Charles Msonde akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa Elimu wa Mikoa, Halmashauri na Waratibu wa Mafunzo ya MEWAKA mara baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo hayo.

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • MAONESHO YA NANENANE July 27, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • WAKULIMA WA MPUNGA KUNUFAIKA NA MRADI WA FTMA

    March 23, 2023
  • RAS MOROGORO AISHAURI TBA, AWATAKA KUFANYA KAZI KWA UFANISI

    March 21, 2023
  • TAASISI ZA KIDINI MOROGORO ZAPONGEZWA KATIKA KULETA MAENDELEO.

    March 20, 2023
  • SERIKALI YASHAURIWA KUTOA FEDHA KUTEKELEZA MIRADI YA UTAFITI

    March 16, 2023
  • View All

Video

Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.