• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAAMUA KUJENGA SEKONDARI

Posted on: February 19th, 2021

.Wananchi wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamekubaliana kujenga Shule mpya tatu za Sekondari zitakazoanza kutumika  mwakani ili kupunguza msongamano wa wanafunzi  katika Shule ya Sekondari ya Mikumi ambayo ndiyo shule pekee katika Mji huo.

Makubaliano hayo yamefikiwa hivi karibuni na wananchi wa Kata ya Mikumi walipotembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa ziara ya kikazi katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi ambapo alifanya kikao na wananchi wa kata hiyo kwa ajili ya kuweka mikakati ya ujenzi wa Shule hizo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao akiwemo Gladness Lukumayi Mkazi wa Mikumi kijiji cha Ihombwe amesema hatua hiyo ya kutaka kuenga shule mpya inatokana na wanafunzi walio wengi kutembea umbali mrefu kutoka wanakoishi hadi Shule ya Sekondari ya Mikumi hivyo kupelekea wanafunzi wengi kupata changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na  wanafunzi wa kike kupata mimba na kupoteza haki zao za kupata Elimu.

Naye Elius Edward Mkazi wa kijiji cha Msimba amesema changamoto wanazokumbana nazo wazazi katika kuwasomesha wanafunzi hao ndio zinazopelekea wananchi kuwa na hamasa ya kujenga Shule katika kijiji chao ili kuepukana na  gharama za usafiri wa kila siku.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ametoa pongezi kwa wananchi wa Mji huo kwa kufikia muafaka wa ujenzi wa Shule za Sekondari tatu kisha kuwataka wananchi hao kuchangia michango ya ujenzi wa Shule hizo ili kuweza kuepukana na changamoto mbalimbali walizozitaa ikiwa ni pamoa na wanafunzi kukaa katika vyumba vya kupanga maarufu kama mageto.

Loata Sanare amebainisha kuwa zaidi ya wanafunzi 1120 Mkoani humo wamesitisha masomo katika kipindi cha  miaka minne huku Mamlaka ya Mji Mdogo Mikumi ikiongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wa kike kupata mimba wakiwa hawaamaliza masomo yao.

Aidha, Loata Sanare amesema sababu ambazo zimechangia idadi kubwa ya wanafunzi kutoendelea na masomo ni kupata mimba na kutembea umbali mrefu ili kufika Shule ya Sekondari Mikumi ambapo wanafunzi hulazimika kutembea zaidi ya kulometa 30 kila siku kufika Shuleni hapo.

Sambamba na hayo Loata Sanare amekerwa na kitendo cha wanafuzi kukaa katika nyumba za kupanga (GHETTO) akibainisha kuwa ndiyo sababu inayopelekea wanafunzi kupata mimba kutokaka na kutokuwepo uangalizi wa karibu wa wazazi ama walezi kwa wanafunzi hao.

‘’Mtoto anakaa ghetto unajuaje usalama wake, wazazi mnakuwa na amani na kulala salama, mzazi wa hapa mtoto wako wa kike hata wa kiume siku hizi yupo getto hana mzazi ambaye umemuachia umeenda ukampangishia chumba ukamwambia mtoto kaa hapa, ikifika saa moja naye anaenda kufanya shughuli zake’’ amesema Sanare

Katika hatua nyingine Loata Sanare amewataka watendaji wa vijiji  kuwahamasisha wananchi kwa ajili ya ujenzi wa shule hizo huku akitoa onyo kali la kuwachukulia hatua za kisheria mwanacnhi ambaye atapingana na agizo hilo la uchanga fedha kwa aili ya maendeleo ya shule mpya zitakazojengwa katika hapo Mikumi.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.