• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waandishi Morogoro wahimizwa kutoa elimu kwa jamii

Posted on: February 16th, 2024

Wandishi Morogoro wahimizwa kutoa elimu kwa jamii.

Shirika la Childhood Development Organization (CDO) limetoa mafunzo kwa Waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro kuhusu Sayansi ya Malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ili kuwa na uelewa na kuweza kupeleka elimu hiyo katika jamii zinazowazunguka.

Mafunzo hayo kwa waandishi wa habari yametolewa Februari 16, 2024 na Mratibu  wa Shirika la CDO Bw. Innocent Rusumyo kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Bw. Innocent amesema kuwa Shirika hilo limepewa dhamana na Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro pamoja na wadau kuratibu utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT – MMMAM) Mkoani humo.

Aidha, ameeleza kuwa kupitia Mradi wa Mtoto Kwanza ambao unalenga kusukuma utekelezaji wa program hiyo ngazi ya mikoa hushirikisha Waandishi wa Habari kama wadau muhimu katika kuripoti, na kuibua ajenda zinazohusu masuala ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto katika jamii, hivyo wametoa mafunzo hayo kwa waandishi hao ili waweze kuipeleka elimu hiyo kwenye jamii.

“...Baada ya mafunzo haya jamii zetu hasa za Mkoa wa Morogoro ambao zinasikiliza vyombo mbalimbali vya habari wanaweza kupata uelewa juu ya kumlea mtoto akiwa na umri wa mwaka sifuri hadi miaka nane….” Amesema Bw. Innocent.


Katika hatua nyingine, Mratibu huyo amebainisha kuwa tafiti zinaonesha kuwa asilimia 43 ya watoto wa miaka sifuri hadi miaka nane wapo katika hatari ya kutofikia ukuaji timulifu, hivyo Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuanzisha program hiyo ambayo inagusa maeneo matano ambayo ni lishe bora, Afya, ujifunzaji wa awali, ulinzi na usalama pamoja na malezi yenye muitikio.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi. Felistas Kalomo amewahimiza wanaume Mkoani humo kuacha tabia ya kuwatelekeza wanawake pindi wanapokuwa wajawazito na kuwataka kushirikiana katika kipindi cha ujauzito na pale mwanamke anapojifungu.


Naye mwakilishi wa Waandishi wa habari waliopata mafunzo hayo Mwajuma Rambo amesema watakuwa bega kwa bega katika kufikisha elimu kwa jamii inayowazunguka ya namna bora ya malezi na makuzi kwa watoto na kwa jinsi gani wazazi wanatakiwa kulea watoto ili waweze kukua katika afya iliyo bora.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.