• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waathirika wa mafuriko Kilosa wapatiwa msaada wa milioni 50.

Posted on: December 13th, 2023

Waathirika wa mafuriko Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamepatiwa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 50 kwa lengo la kuwasaidia walioathirika zaidi na mafuriko hayo ili waweze kujikimu kimaisha wakati Serikali ikiendelea kufanya tathmini ya kina.

Akikabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka, Disemba 12, 2023, Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima amesema wananchi zaidi ya 4700 wameathiriwa na mafuriko hayo huku nyumba 997 zilizingirwa na maji kati ya hizo nyumba 85 zimesombwa na maji kabisa.

"...hiki tulichokusanya ndiyo hicho hicho tunapeleka Kilosa hadi sasa sisi Mkoa... tumekusanya mali zenye thamani ya shilingi milioni 50...” amesema Mhe. Adam Kighoma Malima.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema mafuriko hayo yamesababisha uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo madaraja manne, Barabara na mashamba vyakula na mali nyingine huku watu wawili wakiripotiwa kufariki kutokana mafuriko hayo.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amerudia maelekezo aliyoyatoa hivi karibuni kwa wananchi wa kilosa kutodharau ushauri wa wataalam wa kutorudi kwenye nyumba zao bila kujiridhisha kwa wataalam hao  hususan zilizothiriwa sana na mafuriko huku akibainisha kuwa nyumba hizo haziko salama kwa kuwa zimenyonya maji mengi  na muda wowote zinaweza kuanguka na kuleta madhara makubwa.

Sambamba na agizo hilo Mhe. Malima ameishukuru Serikali, wadau mbalimbali wa maendeleo na chama cha mapinduzi kwa kuungana pamoja katika kuwasaidia wananchi wa Kilosa waliokumbwa na kadhia hiyo ya mafuriko.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka ameishukuru Serikali kupitia Mkuu wa Mkoa, Kamati za ulinzi na usalama za Mkoa na Wilaya pamoja na wadau waliotoa misaada hiyo na kwamba Serikali inawajali wananchi wake.

Aidha, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha shilingi bilioni 13 kwa ajili kuboresha miundombinu ndani ya Wilaya hiyo kwa lengo la kupunguza maafa huku akibainisha kuwa waathirika hao bado wanauhitaji wa misaada hivyo amewaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia waathirika wa mafuriko hayo.

Naye Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati Bi. Janeth shango kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa benki hiyo ametoa pole kwa wananchi waliyoathirika Wilayani Kilosa ambapo benki hiyo imetoa shilingi milioni 10. 

Bi.Janeth amebainisha kuwa Benk hiyo ina utaratibu wa kutoa kwa wananchi sehemu ya faida wanayoipata hususan kwa waliopatwa na matatizo mbalimbali ili kuungana na Serikali katika kupunguza matatizo kwa wananchi hao. 

Akizungumza kwa niaba ya chama cha mapinduzi mkoani humo, Katibu wa Chama hicho ndg. Solomon Kasaba amemshukuru Mkuu wa Mkoa huo na Mkuu wa wilaya ya Kilosa na Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na wadau waliojitokeza kutoa misaada kwa waathirika wa mafuriko wilayani kilosa  na akatumia fursa hiyo kutoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kutoa misaada kwani bado uhitaji ni mkubwa. 

Misaada iliyotolewa kwa waathirika wa mafuriko Wilayani Kilosa ni pamoja na vifaa vya ndani kama sufuria, ndoo, masinia mashuka, sahani na bakuli. Vingine ni vyakula kama mchele, unga wa sembe, mafuta ya kupikia, maharagwe na sukari.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.