• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WADAU WASHAURI MALEZI BORA KWA WATOTO

Posted on: November 18th, 2022

Kutokana na kuongezeka kwa matukuio ya ukatili kwa Watoto hapa nchini wadau wa maendeleo washauriwa kuongeza ushirikiano katika suala zima la malezi bora kwa Watoto kwa kuwa ndio Taifa la kesho.

Ushauri huo umetolewa Novemba 18, mwaka huu na Bi. Peris Lumambo Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wakati akichangia hoja kwenye kikao cha mapitio ya Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto kilicho fanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Afisa Ustawi wa Jamii amesema matukio ya ukatili dhidi ya Watoto yanaongezeka siku hadi siku hivyo ametoa wito kwa wadau, wazazi, Serikali na makundi yote katika jamii kuongeza nguvu katika malezi ya Watoto ili kujenga jamii yenye maadili mema.

“...wito wangu kwa sekta zote idara ya afya, ustawi wa jamii, lishe, elimu, maendeleo ya jamii lakini tukishirikiana na jeshi la Polisi kupitia Dawati la Jinsia na watu wa Mahakama tushirikiane katika suala zima la malezi kwa sababu sasa hivi hali ni mbaya...” amesema Bi. Peris Lumambo.

Aidha, Bi. Peris Lumambo amesema kuwa matukio mengi ya ukatili kwa Watoto kama vile ulawiti, ubakaji na vitendo vingine vinafanywa na ndugu wa karibu, hivyo wazazi wanatakiwa kuwa karibu na Watoto wao ili kupunguza ukatili huo.

Sambamba na hilo Afisa Ustawi wa Jamii amewashauri wamiliki wa shule za Watoto wadogo ‘Day Care’ kuunda umoja wao na kupatiwa elimu ya malezi bora kwa Watoto ili kujenga jamii bora kwa kuwa wao muda mwingi wanakuwa na Watoto hao.

Kwa upande wake Bi. Felistas Kalomo Mkurugenzi Mkuu Shirika la Maendeleo ya Mtoto (CDO) amesema suala la malezi linawahusu wazazi wote wawili baba na mama ili kumjenga mtoto katika maadili yanayofaa katika jamii zetu, kulega lega kwa wazazi katika majukumu yao ya ulezi wa familia kunasababisha Watoto kuharibikiwa kimaadili, ameongeza kuwa wazazi wanawajibu wa kuangalia usalama wa watoto wao ili kubaini changamoto zinazo wakumba Watoto.

Akihitimisha kikao hicho Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio amesema kikao kijacho kunahaja ya kushirikisha wadau mbalimbali ambao kwa kiasi kikubwa wanahusika na suala la malezi na maadili kwa Watoto ili kuongeza ufanisi katika mapambano dhidi ya ukatili kwa Watoto na kujenga malezi bora kwa jamii.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.