• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wafanyabiashara ndogondogo kunufaika na vitambulisho vya kidijitali.

Posted on: February 20th, 2024

Wafanyabiashara ndogondogo kunufaika na vitambulisho vya kidijitali.

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuja na mfumo mpya wa kuwasajili wafanyabiashara ndogondogo na kuwapatia vitambulisho vya kidijitali kwa lengo la kuwatambua, kupata takwimu sahihi na kuwapa mazingira rafiki ya kufanyia biashara wafanyabiashara hao.

Hayo yamebainishwa Februari 20, 2024 na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro  Bi. Neema Dachi wakati akifungua kikao cha mafunzo kwa Maafisa Biashara, Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa TEHAMA kutoka Halmamshauri zote za Mkoa huo kilichofanyika ukumbi wa Chifu Kingalu uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akibainisha zaidi Bi. Neema Dachi ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Usimamizi wa Serikali za Mitaa ametaja faida watakazopata wafanyabiashara hao mara baada ya kujisajili na kupata vitambulisho hivyo vya kidijitali kuwa ni pamoja na Kutambulika na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kutambulika na Jeshi la Polisi pamoja na kutambulika  kwenye Ofisi za Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri.

Aidha, Bi. Neema amesema vitambulisho hivyo ambavyo wafanya biashara ndogondogo wanahimizwa kuwa navyo vitawasaidia katika kutunza fedha na kufanya mihamala mbalimbali ya kifedha pamoja na kuunganishwa na mifuko ya kijamii kama vile NSSF.

“….Serikali imeamua kuja na mfumo wa kidijitali ili kuwatambua wafanya biashara ndogondogo na itawasaidia kufanya biashara zao pasipo kubugudhiwa….” amesema Bi. Neema.

Katika hatua nyingine  Kaimu Katibu Tawala huyo wa Mkoa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wafanyabiashara ndogondogo kwa kutoa fedha kutoka Hamlashauri za Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya ujenzi wa maeneo ya kufanyia biashara zao.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii kutoka Wizara ya Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Bw. David Malebetho amewataka wafanyabiashara ndogondogo Mkoani humo kujitokeza kwa wingi na kujisajili ili kupata vitambulisho hivyo na kuondokana na changamoto zinazowakabili zikiwemo za kutofahamika na kutokuwa na maeneo sahihi na salama ya kufanyia biashara zao hivyo kupelekea kuzagaa katika maeneo mbalimbali bila mpangilio na kukosa uhuru wa kufanya biashara zao.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.