• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wafanyabiashara watakiwa kujiepusha na matumizi ya mifuko ya plastiki, watakaobainika kufikishwa Mahakamani.

Posted on: September 17th, 2022

Wafanyabiashara watakiwa kujiepusha na matumizi ya mifuko ya plastiki, watakaokaidi kufikishwa mahakamani.

Serikali Mkoani Morogoro imewaagiza Wadau na wananchi wote kujiepusha na matumizi ya mifuko ya plastiki pamoja na mifuko mbadala isiyokidhi ubora na viwango vilivyoainishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na kwamba watakaokaidi agizo hilo watafikishwa Mahakamani.

Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa adhara uliofanyika nje ya soko kuu la Chifu Kingalu Morogoro.

Agizo hilo limetolewa Septemba 17 mwaka na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Aboubakar Mwassa alipotembelea soko la Chifu Kingalu lililoko katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa lengo la kuwakumbusha wafanyabiasha kujiepusha na matumizi ya mifuko hiyo lakini pia kusikiliza kero za wafanyabiashara wa soko hilo.

Akibainisha kuhusu matumizi ya mifuko ya Plastiki, Fatma Mwassa amesema mojawapo ya vigezo vya mifuko inayoruhusiwa kutumika kwa mujibu wa TBS ni pamoja na mifuko hiyo iwe na anwani na jina la mzalishaji, iwe na alama za urejelezaji, iwe imethibitishwa ubora wake na TBS na iwe na unene usiopungua microns 30 kwa upande mmoja, au Microns 60 kwa pande zote mbili.


Mkuu wa Wilaya ya manispaa ya morogoro Albert Msando akizungumza na wananchi waliohudhuria mkutano.

Kwa upande wa mifuko mbadala mifuko hiyo iwe na jina na anwani ya mzalishaji, iwe na alama au maneno ya urejelezwaji iwe na uzito usiopungua gramu 70,ioneshe uwezo wake wa kubeba na ubora wake uwe umethibitishwa na TBS.

Kwa mujibu wa kanuni ya 8 kifungu kidogo A mpaka E ya kanuni za usimamizi wa mazingira za kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki ya mwaka 2019,inaeleza kuwa mtu yeyote akikutwa anatumia mifuko ya plastiki isiyo na ubora na kukutwa na hatia anatakiwa kufikishwa mahakamani.

“mtu yeyote atakayeingiza au kusafirisha nje ya nchi au kuzalisha au kuuza au kuhifadhi au kusambaza au kumiliki au kutumia mifuko na vifungashio vya plastiki kinyume na kanuni, atakuwa ametenda kosa na endapo atatiwa hatiani kulingana na kosa anaweza kufikishwa mahakamani” amesema Fatma Mwassa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akizungumza na Wananchi waliohudhuria mkutano wa adhara

Agizo hilo la Fatma Mwassa la kutotumia mifuko ya plastiki na vifungashio visivyo na ubora linakuja ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokomeza mifuiko hiyo isiyokuwa na ubora na kukumbushwa na Dkt. Suleman Jafo Waziri wa Nchi  Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira alipozungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma Agosti 26, 2022.

Meneja wa kanda Morogoro Rufiji NEMC Amina Kibola akitoa maelekezo ya madhara ya mifuko ya plastiki isiyokidhi viwango na ubora kwa wananchi

Katika hatua nyingine Fatma mwassa akiwa katika soko hilo ametatua baadhi ya kero za wananchi ikiwa ni pamoja na malalmiko ya ufujaji fedha za makusanyo katika soko hilo ambapo Mkuu huyo ameelekeza kuwa kuanzia sasa fedha zote zinazokusanywa katika soko hilo zilipwe kupitia Control number ili kudhibiti upotevu wa fedha hizo za Serikali.

Aidha, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro ashirikiane na wataalamu wake kufanya upya uchaguzi wa Viongozi wa Soko hilo ili kupata viongozi wapya badala ya kubaki na viongozi wanaolalamikiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akikagua Mabanda ya wamachinga soko kuu la Chifu Kingalu lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

Akipokea maagizo ya Mkuu wa MKoa, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando amesema anakwenda kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na kiongozi wake huku akiahidi mbele yake kuwa uchaguzi wa viongozi wa Soko la Chifu Kingalu utafanyika kwa huru na haki.\

Akizungumzia kuhusu mifuko ya plastiki, Meneja wa Kanda ya Morogoro - NEMC Amina Kibola amewaasa watanzania kutumia mifuko ya vikapu badala ya mifuko ya plastiki kwa kuwa amesema mifuko hiyo ina madhara makubwa kwa binadamu, wanyama na udongo pamoja na kuharibu mazingira kwa kuwa mifuko hiyo haiozi na inakaa hadi miaka 500 ardhini jambo ambalo ni hatari kwa vizazi vya baadae.

Muonekano wa soko kuu la Chifu Kingalu lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

Kwa upande wao wananchi akiwemo Philip Msangi Mkazi wa Morogoro na mfanyabiashara wa soko la Chifu Kingalu yeye anapinga kubomolewa kwa vibanda vya biashara vilivyojengwa sokoni hapo kwa hoja kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika vibanda hivyo, anashauri kuweka barabara kila baada ya vibanda hivyo lengo kila mfanyabiashara aonekana lakini sio kuvibomoa vibanda vyote.

Kuhusu mifuko ya plastiki Bw. Msangi anasema kwa sasa kila mwananchi anajua kuwa mifuko ya plastiki imepigwa marufuku na Serikali na kila mmoja anajua athari zake na kwamba wanaoingiza au kutumia wanakaidi tu na kuiomba serikali iwachukulie hatua kali.

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.