• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAFUGAJI MVOMERO WAPONGEZWA, WATAKIWA KUCHANGIA MAPATO YA HALMASHAURI.

Posted on: June 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewapongeza wafugaji wa Wilaya ya Mvomero kwa kuwa na mchango mkubwa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Mhe. Malima amesema hayo Juni 13 mwaka huu wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG Wilayani MVOMERO.

Mhe. Adam Malima akisalimiana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi - CCM akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho Wilayani Mvomero Ndg. Michael Jaka na Alhaj Sengulo .

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, amefurahishwa sana kuona sekta ya mifugo katika Halmashauri hiyo inachangia kwa asilimia kubwa ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia Sekta ya Mifugo

Eneo la mnada wa mifugo uliopo Wilayani Mvomero.

Akisisitiza ukweli huo Mhe. Malima amesema,  Halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ilifanya makisio ya kukusanya mapato kupitia Sekta ya mifugo na kukusanya shilingi 392,854,000 na kufanikiwa kukusanya jumla ya shilingi 405,624,177 sawa na 103%.

“...sasa nakuambieni wanamvomero, katika Wilaya peke yake ambayo nimeona kidogo ina mchango wa kuridhisha wa wafugaji ni Mvomero...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Kwa sababu hiyo amewataka wafugaji katika wa Halmashauri  nyingine za Mkoa huo kuiga Mfano huo wa wafugaji wa Mvomero kuwa na mchango wa ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri kupitia mifugo yao badala ya kuwa kero kwa jamii na kwa Halmashauri  yenyewe.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Malima amewataka Wahe. Madiwani wa Halmashauri hiyo kuweka utaratibu wa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao kwa kuwa wao ndio wasimamizi wakuu wa miradi hiyo, hivyo amewataka kuunda kamati itakayofuatilia miradi ya maendeleo.

Baadhi ya Wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Mvomero wakiwa kwenye mkutano wa baraza la Madiwani.

Nae Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu Bw. Anza Ameni Ndosa kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo amewakumbusha Wahe. Madiwani pamoja na watendaji wa Halmashauri hiyo kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo kikamilifu na kwa kufanya hivyo miradi hiyo itakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu Bw. Anza Ameni Ndosa (kulia) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa ambaye ni kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mvomero.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Yusuph Makunja amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwa na nia njema ya kuibadilisha Halmashauri hiyo na kuwapa nguvu madiwani hao katika usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mvomero Mhe. Yusuph Makunja (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri hiyo Bw. Linno Mwageni wakati wa mkutano wa baraza la Madiwani.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akikagua miundombinu ya barabara Wilayani Mvomero.

Pichani ni baadhi ya majengo ya shule ya sekondari ya Sokoine Memorial.

Muonekano wa jengo la dharura katika hospitali ya Wilaya ya Mvomero.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.