• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wahanga wa Mafuriko Kilosa kupatiwa msaada.

Posted on: December 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Kamati za Maafa za Mkoa na Wilaya ya Kilosa itatoa msaada wa chakula, magodoro, mashuka na mavazi kwa wahanga wa mafuriko yaliyotokea usiku wa kuamkia Disemba 5 mwaka huu na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku baadhi ya familia zikikosa mahali pa kuishi.

Mhe. Malima amebainisha hayo Disemba 6 mwaka huu wakati akizungumza na wananchi wa Vijiji vya Rudewa na Mvumi Wilayani Kilosa kwenye ziara yake ya kutoa pole kwa wahanga na kuangalia maeneo yaliyoathirika na mafuriko hayo.

Mhe. Malima ametoa pole kwa familia iliyoondokewa na mpendwa wao pamoja na wahanga waliopoteza makazi yao kutokana na mafuriko hayo huku akibainisha kuwa Ofisi yake kwa kushirikiana na kamati ya Maafa ya Wilaya ya Kilosa itatoa msaada huo vikiwemo vyakula na mahitaji muhimu.

"...nimekuja kuwaona ndugu zangu wa Mvumi na Rudewa baada ya janga ambalo limetukuta jana lakini jambo kubwa ni kupeana pole kwa niaba ya Dkt. Samia na Serikali yake lakini Kwa hatua ya kwanza kwa wale waathirika tuone tunafanya nini..." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mkuu wa huyo wa Mkoa amewaagiza Mameneja wa Wakala ya Barabara Vijijini - TARURA, Shirika la Umeme - TANESCO na Wakala wa Maji safi na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA Mkoani humo kufanya tathmini na maboresho ya miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko hayo ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za umeme, maji na Barabara kama ilivyokuwa awali.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Malima amewataka baadhi ya watu kuacha tabia ya kuwaibia wengine pindi maafa yanapotokea huku akisema kuwa Serikali itawachukulia hatua za kisheria wale wote waliojihusisha na wizi wa mali wakati wa zoezi la uokoaji likiendelea ambapo watu watatu wanashikiriwa na Jeshi la Polisi Wilayani hapo kwa kuiba mali za wahanga wa mafuriko.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema Jeshi la Polisi Wilayani hapo limejiandaa kukomesha vitendo vyote vya kiharifu ambapo kwa sasa Jeshi hilo linaendesha Kampeni ya kutokomeza uharifu na madawa ya kulevya, hivyo halitafumbia macho viashiria vyovyote vya uharifu na uvunjifu wa amani Wilayani humo na kuahidi kuwa Jeshi litahakikisha kuwa waliohusika na wizi wakati wa maafa wanachukuliwa hatua za kisheria.

Nao baadhi ya Wahanga wa Mafuriko hayo akiwemo Bw. Mohammed Twahibu ambaye nyumba yake imesombwa na maji amesema chanzo cha maji kuzingira nyumba za watu ni kukosekana kwa tuta la kuzuia maji kuingia kwenye makazi ya watu, hivyo ameiomba serikali kufanya maboresho ya kingo za mto Mvumi ili kuepusha athari zaidi kwa siku zijazo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ametembelea maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo hususan Vijiji vya Rudewa na Mvumi na kuzungumza na wananchi na kuwataka kuwa watulivu wakati huu, huku Serikali ikiendelea kufanya tathmini zaidi na kutoa wito kwao kuendelea kuchukua tahadhari za mvua zinazoendelea kunyesha hapa mkoani.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.