• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

Posted on: March 3rd, 2021

Wahasibu wa Halmashauri za Serikali za Mitaa Mkoani Morogoro wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata Sheria, Taratibu, Kanuni, Maadili ya kazi zao ili kuepuka kupoteza nafasi hizo kwa kwenda kinyume na maadili ya kazi zao ikiwa ni pamoja na kutoa nywila za mfumo wa malipo Serikalini - MUSE.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo alipokuwa akifungua mafunzo ya mfumo wa Malipo Serikalini - MUSE kwa Wahasibu wa Halmashauri, maafisa Manunuzi na Maafisa TEHAMA yaliyofanyika mwanzoni mwa wiki hii katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mhandisi Kalobelo amewataka na kuwaonya wahasibu katika kikao hicho kutothubutu kutoa nywila za mfumo huo kwa mtu asiyehusika kwani kufanya hivyo ni kukiuka maadili na sheria za kiutumishi na atakaebainika atakuwa sehemu ya uharifu pindi itakapobainika kuna tatizo kwenye mfumo huo katika  ya Ofisi yake.

‘’Nisisitize kwa waweka hazina, kumekuwepo na tabia kwamba password unazopewa unagawa kwa mtu mwingine ambaye hana ethics za kutumia huo mfumo, wewe umefundishwa na unajua madhara ya kutoa password kwa mtu mwingine, sasa nawaomba hizo password mtakazopewa ziwe zako mwenyewe kwa majukumu yako’’ alisisitiza Mhandisi Kalobelo.

Sambamba na hayo, Mhandisi Kalobelo amewataka washiriki wa kikao hicho  kushiriki kikamilifu kwa kuwa watulivu, wasikivu  na wavumilivu ili kujengeana uelewa na kufanyakazi kwa vitendo katika mafunzo hayo.

Akibainisha umuhimu wa matumizi ya mfumo wa MUSE, Afisa Hesabu kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI  Idara ya TEHAMA Kitengo cha Usimamizi wa Mifumo ya Fedha Bi. Catherin Uyoga amesema lengo la kikao hicho ni kuwajengea uwezo wahasibu wa Halmashauri, Maafisa TEHAMA na Maafisa Ununuzi ili ifikapo Julai mwaka huu Halmashauri zote Tanzania zianze kutumia mfumo huo, hivyo kuwawezesha kufanya malipo ya fedha za Serikali na malipo mengine kwa wananchi bila kukwama.

amesema MUSE imetengenezwa baada ya changamoto zilizojitokeza katika mifumo  mingine ya Serikali kutokidhi mahitaji pamoja na kugharimu fedha nyingi katika kuitumia ukiwemo mfumo wa EPICA, kwa sababu ni mfumo kutoka nje ya nchi hivyo Serikali kuamua kuunda mfumo wa MUSE ambao tayari baadhi ya taasisi za Serikali zimekwisha anza kuutumia.

Naye, Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro Bi. Flora Rajab amesema mfumo huo utawasaidia katika kusimamia Halmashauri za Mkoa huo lengo kuu ni kuziwezesha kufanya usuluhishi wa mahesabu ya fedha kila mwezi, uchukuaji wa masurufu, uandaaji wa taarifa za mwezi, utoaji wa taarifa za robo mwaka na taarifa za mwisho wa mwaka kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bi. Margareth Nembo amesema MUSE imetengenezwa baada ya kutokea changamoto nyingi ndani ya mifumo  iliyokuwepo kwani mfumo wa MUSE ni mzuri kutokana na kutotumia gharama kubwa ukilinganisha na mfumo wa EPICA kutoka nje ya nchi hivyo kutumia ghalama kubwa wakati wa uendeshaji.

Mfumo wa Malipo Serikalini yaani MUSE ulianza kubuniwa na Wizara ya Fedha na Mipango na kuundwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI baada ya kufanya uchambuzi wa matumizi ya mifumo ukiwemo EPICA na kubaini kuwa Serikali ilikuwa inatumia fedha nyingi sana kugharimia ununuzi, uundaji usimikaji na uendeshaji wa mifumo ya kielektroniki ya usimamizi wa fedha za Umma na kuamua kuchukua hatua ya kuunda mfumo huu mpya wa MUSE hapo Machi, 2019.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.