• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAHUDUMU WA MABASI NCHINI KUTAMBULIWA RASMI NA SERIKALI.

Posted on: March 19th, 2024

WAHUDUMU WA MABASI NCHINI KUTAMBULIWA RASMI NA SERIKALI.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebecca Nsemwa amesema Serikali kupitia chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kwa kushirikiana na Mamlaka ya udhibiti na usafiri wa ardhini (LATRA) Wameanza kuwatambua rasmi watoa huduma za mabasi ya masafa marefu na mijini kwa kuwapatia mafunzo yatakayowasaidia kuongeza weledi katika utendaji kazi ndani ya sekta hiyo ya usafirishaji.

Mhe. Rebecca ameyasema hayo Machi 18, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku tano katika ukumbi wa mikutano za Ofisi ya TAFORI zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kubinisha kuwa Wizara ya Uchukuzi na Wizara Elimu  Sayansi na Teknolojia waliwezesha kuwepo mradi wa East Afrika Skills for Transportation and Regional Intergration Project ambapo unafadhiliwa na Benki ya Dunia (World Bank) lengo ni kuwafanya watoa huduma ya mabasi kutambulika na Serikali.

“…Ndugu zangu nimefurahi sana kwa kujali kada hii ya uhudumu wa mabasi ya masafa marefu na mjini kwa kurasimisha kada hii kuwa kada inayotambulika na Serikali….” Amesema Rebecca Nsemwa.

Pia Mkuu huyo wa Wilaya amekipongeza Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na Malaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini(LATRA) kwa kufikia hatua ya kutoa mafunzo kwa Wahudumu wa mabasi ambapo itawasaidia kutoa huduma bora kwa kuzingatia sheria na taratibu zote za utoaji huduma.

Katika hatua nyingine Mhe. Rebeca Nsemwa ametoa wito kwa viongozi wa chuo cha Taifa cha Usafirishaji kuwa wabunifu na kufanya kazi kwa weledi ili kukifanya chuo hicho kuwa mahala sahihi pakupatia mafunzo mbalimbali.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) anayeshughulikia Utawala na fedha Bi.Zainabu Mshana amesema mafunzo hayo yataongeza hali ya usalama wa abiria na mali zao na kwamba yatakua ni endelevu, hivyo amewataka watu kuchangamkia fursa ili kujitokeza kwa wingi kujiunga na Chuo hicho katika Taamula hiyo ya Uhudumu wa Mabasi.

Naye Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhiti na Usafiri Ardhini (LATRA) Bw.Andrew Mlacha amebainisha kuwa kupitia mafunzo yanayotolewa watapata takwimu sahihi zitakazowawezesha kuwatambua rasmi watoaji huduma katika mabasi ya masafa marefu na mijini.

Naye Filbert Othman akiongea kwa niaba ya wenzake wanaopata elimu hiyo ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali na kuweza kuwapatia elimu ambayo ni muhimu na itawasaidia kutambulika na kupata haki zao kama wafanya kazi wengine.

Mafunzo hayo ya siku tano, tayari yametolewa katika baadhi ya Mikoa ikiwemo Kilimanjaro, Mbeya na  kwa sasa yanatolewa katika Mkoa wa Morogoro ambapo jumla ya washiriki 73 wamejitokeza kupata mafunzo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.