• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUZALISHA BIDHAA ZENYE UBORA.

Posted on: May 29th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Albinis Mgonya amewataka wajasiriamali Mkoani Morogoro kuzalisha bidhaa zenye ubora kisha kihakikisha zinathibitishwa na Wakala wa Viwango Tanzania - TBS ili kuleta ushindani katika soko la ndani nanje ya nchi.

Mhe. Mgonya ametoa kauli hiyo Mei 29, 2021 katika Uzinduzi wa mafunzo ya kusherekea kilele cha kutimiza miaka 10 ya kuanzishwa kwa Taasisi ya GS1 Tanzania ambayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

‘’TBS Endeleeni kutoa Elimu kwa wakulima na wazalishaji kuhakikisha kwamba wanazingatia viwango vilivyowekwa ili kuzalisha kwa ubora, na tunapotoa Elimu inarahisisha wanapoenda kupata kibali kwenye mamlaka husikawatazingatia vigezo ambavyo vinatakiwa’’ Amesema Mgonya.

Aidha, Mhe. Mgonya amebainisha umuhimu wa Msimbomilia katika bidhaa ni kumsaidia mlaji na wadau wengine kutambua mahali bidhaa ilipozarishwa, kutambua kama bidhaa imethibitishwa na TBS, kusaidia kutambua namna ambavyo bidhaa imetengenezwa na kusaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa kutambua bidhaa zinazozarishwa kwenye kwenye maeneo yao.

Kwa upande wake Afisa Ufundi wa GS1 Tanzania Ndg. Killian Charles  ametoa wito kwa wajasiriamali kuweka Msimbomilia katika biashara zao ili kuzisaidia biashara hizo kufika katika masoko makubwa bila kuwepo usumbufu wowote katika masoko ya ndani na nje.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Asha Rajabu amesema kupitia hutuba ya mgeni rasmi atahakikisha biashara zake anazisajiri TBS na kuhakikisha zinakuwa na Msimbomilia ili kufanya ushindani katika Masoko,

GS1 Tanzania ni Taasisi iliyoanzishwa kwa juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia shirika la utafiti na maendeleo ya viwanda (TIRDO) chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Taasisiya sekta binafsi  (TPSF)  kwa jukumu la kuziwesha bidhaa za Tanzania kupata utambulisho wake wa alama za mistari Msimbomilia (Barcodes).

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.