• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wajumbe wa bodi ya barabara Morogoro waazimia kuongezewa bajeti.

Posted on: March 4th, 2025

Wajumbe wa bodi ya barabara Mkoa wa Morogoro wameazimia kwa kauli moja kuwasilisha maombi ya kuongezewa bajeti kwa ajili ya Wakala ya Barabara Tanzania (TANROARDS) na Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani humo ili kufanikisha ujenzi wa miundombinu ya barabara ndani ya mkoa huo.


Wajumbe wa Bodi hiyo wameazimia hilo Machi 4, Mwaka huu wakati wa kikao cha 43 cha bodi ya barabara kilichofanyika  ukumbi wa mikutano wa Magadu uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro hoja iliyotokana na ukweli kwamba Mkoa huo ni mkubwa ukilinganisha na mikoa mingi hapa nchini.



Akifafanua zaidi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa huo ni mkubwa huku akitolea mfano kutoka mpakani mwa Namtumbo hadi Gairo ni umbali wa km 800 ukiwa bado ndani ya mkoa hivyo hauwezi kuwa na bajeti sawa na Mikoa mingine kwa sababu ya ukubwa huo.


"...tumejenga hoja TANROARDS na TARURA kwamba Mkoa wa Morogoro muuangalie kwa utofauti... hebu angalia kutoka Namtumbo hadi Gairo ni km 800 halafu bajeti inafanana na Mikoa mingine lazima watuangalie..." Amesema Mkuu huyo wa Mkoa.


Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amekemea vikali mwananchi aliyeharibu barabara kwa kulima zao la mpunga sehemu ya kipande cha barabara na kuleta taharuki kwa wananchi wengine na kuharibu barabara hiyo hivyo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro kushughulikia haraka kadhia hiyo kabla ya Machi 8, Mwaka huu ili siku ya tarehe hiyo atakapotembelea asikute uharibifu huo na hatua ziwe zimechukuliwa kwa mhusika.


Sambamba na hayo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka TANROARDS na TARURA kuweka alama za barabarani kwa maeneo yote yanayostahili kuwekewa alama ili kusaidia usalama kwa wasafiri na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali yakiwemo mazao.


Kwa upande wake, Meneja wa TANROARDS   Mkoa wa Morogoro Mhandisi John Mkumbo  amesema TANROARDS inasimamia barabara zenye urefu wa km 6406.69 kati ya hizo km 100.07 ni za kiwango cha lami, km 1487.3 ni za changarawe na km 4,819.28 ni za udongo.


Amesema miradi hiyo ya maendeleo inayotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa kiwango cha lami kwa kipande cha Ifakara - Taweta - Madeke, ujenzi wa daraja la duthumi ( barabara ya bigwa kisaki), ujenzi wa kiwango cha lami Gairo Pr. school njia panda ya malimbika hospitali, ujenzi wa kiwango cha lami eneo la chuo cha mzumbe barabara ya Sangasanga - langali utekelezaji unaendelea, na ukarabati wa barabara ya Mvomero - Ndole - Kibati pia utekelezaji unaendelea.


Naye, Meneja wa Wakala ya Barabara ya Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Emmanuel Ndyamkama amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 TARURA Mkoani humo imepanga kutumia kiasi cha Tsh. Bil. 24.9 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara kwa kupitia vyanzo vya fedha za mfuko wa barabara,  mfuko wa jimbo na fedha za tozo.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.