• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKADILIAJI MAJENZI KUONGEZA UFANISI KATIKA MIUNDOMBINU.

Posted on: October 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema wakadiliaji majenzi wamekuwa nguzo katika utoaji wa thamani ya miundombinu mbalimbali ikiwemo miradi ya barabara, maji, elimu na afya ili kukadiria miradi hiyo kabla ya kuanza ujenzi ili kuepuka matumizi makubwa ya fedha za Serikali.

Mhe. Malima amesema hayo Oktoba 10, Mwaka huu kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (MB) katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa 30 wa wakadiliaji majengo na semina ya mafunzo kwa wataalam wa ujenzi ikiwa na lengo la kuwajengea uwezo maafisa ukadiliaji hao.

Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema wakadiliaji majenzi ndio wanapaswa kufanya makadirio ya miradi ili kuwa na miradi itakayolingana na fedha zitakazotolewa (value for money) na kuondoa changamoto ya kumalizika fedha kabla mradi kuisha.

"... ninyi mnaona suala la ujenzi mimi naona suala la kiuchumi kwenye value for money kwamba msipofanya kazi yenu hakuna value for money... " amesema Mhe. Adam Kighoma Malima 

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wakadiliaji majenzi kujiimarisha katika matumizi ya teknolojia kwa kuongeza elimu na maarifa ili kuendana na wakati uliopo kwani teknolojia mpya zitafanya kupata miundo ya majengo mbalimbali ya kisasa.

Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Wakadiliaji Majenzi cha Tanzania Qs. Bernard Ndakidemi amesema mwaka 2023/2024 Serikali imeajiri wakadiliaji majenzi 200 katika taasisi za ujenzi na kuiomba Serikali kupitia Wizara ya ujenzi kuwashirikisha wakadiliaji majenzi katika miundombinu ili kupata thamani halisi ya miradi na kuepuka upotevu wa fedha za umma.

Naye, Mkurugenzi wa Huduma na Ufundi wa Umeme kutoka Wizara ya Ujenzi Qs. Mwanahamisi Kitogo amesema Serikali kupitia Wizara ya ujenzi imefanikiwa kufanya marekebisho ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiliaji majenzi kuingia katika mfumo wa ajira Serikalini kwani mabadiliko hayo yamelenga kuongeza utendaji kazi wa kitaalamu katika miradi ya umma.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.