• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKAGUZI WA MKOA, HALMASHAURI NA WAKURUGENZI WAPEWA NENO ZOEZI LA ANWANI ZA MAKAZI

Posted on: April 29th, 2022

Wakaguzi wa ndani Mkoa wa Morogoro wametakiwa kushirikiana na wa Halmashauri pamoja na Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri zao ili kuhakikisha zoezi la Anwani za Makazi na Posti Kodi linaloendelea nchi nzima linafanikiwa kama maagizo ya Serikali yalivyoelekezwa.

Ushauri huo umetolewa Aprili 28 mwaka huu na Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Stephen Benedict wakati akifungua mafunzo ya wakaguzi wa Ndani yaliyofanyika katika ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mafunzo hayo ambayo pamoja na kutaka kuwajengea uwezo Maafisa hao kwa ajili ya kutekeleza vema majukumu yao ya kila siku kwenye Halmashauri zao pia yalilenga kushiriki kwa asilimia mia katika kushauri na kukagua matumizi ya fedha za Serikali zilizizoelekezwa kwenye zoezi la Anwani za Makazi na Posti Kodi.

Baadhi ya wakaguzi wa ndani wakiwa kwenye kikao hicho cha siku moja

Hata hivyo amewataka wakaguzi hao watoe ushirikiano kwa viongozi wao katika kutekeleza zoezi hilo kwa ufanisi na sio kusababisha changamoto itakayosababisha kukwamisha zoezi hilo.

“Kwa hiyo twende tukawasaidie waone kwamba sisi ni msaada kwao na sio changamoto…kwa hiyo twende kwenye mlengo huo wa kufikia malengo” amesema.

Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Stephen Benedict (kushoto) akisikiliza kwa makini mafunzo yanayotolewa na Afisa TEHAMA Mhandisi Rhobison Deus (kulia).

Akiongea baada ya mafunzo hayo Mratibu Msaidizi wa Zoezi la Anwani za Makazi na Posti Kodi Mkoa wa Morogoro Kayombe Masoud Rioba  amesema Mkaguzi wa ndani ni jicho la pili la kila taasisi hivyo kuna umuhim wa Maafisa hao kuwepo kwenye zoezi la Anwani za Makazi kwa kila Halmashauri ili kushauri na kusimamia matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya zoezi hilo.

Kwa upande wa zoezi lenyewe la Anwani za Makazi Rioba amesema zoezi hilo linaendelea vizuri na kwa sasa Mkoa huo umejikita kwenye usajiri wa miundombinu na zoezi hilo linategemea kukamilika tarehe iliyopangwa yaani Mei 15 mwaka huu.

wakaguzi wa ndani wakiwa katika picha ya pamoja mara baaada ya kukamilika kikao hicho

Nao wanamafunzo hayo akiwemo Bakari Luguguda Kaimu Mkaguzi wa Ndani Wilaya ya Ulanga amesema kama wadau wanaishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuratibu kikao kazi hicho akibainisha kwamba Kikao hicho kitawasaidia Wakaguzi wa ndani kugagua fedha zinazotumika kwenye zoezi Anwani za Makazi lengo ni sote ka pamoja kukamilisha kwa ufanisi zoezi hilo.

Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa amewataka wakaguzi wa ndani wa Halmashauri zote kufanya kazi kwa uaminifu kama ambavyo Serikali ina wategemea na kuwaona kama jicho la matumizi hayo ya fedha basi wao pia wafanye kazi hiyo inayotazamiwa na Serikali kuanzia kwenye utekelezaji wake hadi kwenye masuala ya matumizi yake.

Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Stephen Benedict akiongea na wakaguzi wa ndani waliohudhuria kikao hicho

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.