• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKAGUZI WA NDANI WATAKIWA KUTOKUWA NA AIBU.

Posted on: March 2nd, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka Wakaguzi wa Ndani Mkoani humo kutokuwa na huruma katika utendaji kazi wao hususan wanapofanya ukaguzi wa fedha na miradi ya maendeleo katika maeneo yao kwa kuwa wao ndio jicho la Serikali.

Dkt. Mussa ameyasema hayo Machi Mosi, 2024 wakati akifunga Kikao Kazi cha Wakaguzi wa ndani wa Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu huyo wa Mkoa.

Katibu Tawala huyo ameeleza kuwa Wakaguzi wa ndani hususan wa Halmashauri wamekuwa wakifumbia macho ubadhilifu wa fedha unaofanyika kwenye Halmashauri huku akibainisha kuwa hali hiyo inasababisha miradi ya maendeleo kutekelezwa chini ya kiwango ama kutokamilika kwa wakati.

Kwa sababu hiyo Dkt. Mussa amewataka watendaji hao kutokuwa na aibu linapokuja suala la kusimamia ukusanyaji wa mapato kupitia mashine za PoS na kuwataka kutoa taarifa kwa ngazi husika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa - TAKUKURU pindi wanapobaini kuwepo viashiria vya wizi wa fedha au vifaa vya miradi.

"...katika utendaji wetu wa kazi tunaoa aibu, tunaona muhali kutekeleza ule wajibu wetu wa kazi tuliopewa na hatimae mambo yanaharibika..."

Aidha, amewataka Wakaguzi hao kuhakikisha kuwa fedha zinazokusanywa  zinapelekwa benki ili kuepusha wizi unaoweza kutokea.

Katika hatua nyingine Dkt. Mussa amewasisitiza Wakaguzi hao kujijengea utamaduni wa kukagua miradi ya maendeleo ili kujiridhisha matumizi ya fedha na ubora wa miradi hiyo inayotekelezwa katika Halmashauri zao kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuongeza ubora wa miradi hiyo na kuwz na thamani ya fedha zilizotolewa.

Naye Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi Bi. Neema Dachi amesema kikao kazi hicho kimelenga kuwakumbusha Wakaguzi wa Ndani majukumu yao ya msingi ikiwa ni pamoja na kuwasaidia Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kwenye ukaguzi wa fedha na miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakaguzi wa Ndani Mkoa wa Morogoro Bw. Isaac Mwang'onda kwa niaba ya Wakaguzi waliohudhuria kikao hicho amemshukuru Katibu Tawala huyo pamoja na timu yake kwa kuandaa kikao kazi hicho na kuahidi kwenda kuyafanyia kazi maagizo na maelekezo aliyoyatoa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.