• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKAZI WA KILOSA WATAHADHARISHWA KUHUSU MAFURIKO

Posted on: December 10th, 2023

Wakazi wa mji wa Kilosa wametafadharishwa kwa mara nyingine kuchukua hatua juu ya kuepukana na mafuriko yanayoendelea kuukumba mji huo kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha ndani na nje ya mji wa Kilosa na kusababisha athari kubwa ya miundombinu, makazi, vyakula na hata kugharimu maisha ya watu.

Wito huo umetolewa Leo Disemba 10, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.Adam Kighoma Malima alipotembelea baadhi ya maeneo yaliyoathirika na mafuriko yaliotokea usiku wa kuamkia leo Disemba 10 katika Kata ya Mkwatani Mtaa wa Manzense B, Wilayani Kilosa Mkoani humo na kutoa pole kwa waathirika.

Mhe. Malima amebainisha kuwa ndani ya siku sita mfululizo, maeneo mbalimbali ya mji  wa Kilosa yamepata athari ya mafuriko, maeneo hayo ni pamoja na Mvumi, Rudewa, Dumila, Kitete na maeneo ya Kilosa Mjini.

“…… Kitu tunachojua ni kwamba Kilosa yetu imekuwa kama bakuli, kwa hiyo maji yote yanayotoka huko milimani ukiongeza na maji yake yenyewe bado inabidi tukae kwa tahadhari kuhusu haya maafuriko….” amesema Adam Malima.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo, kwa mara nyingine kufanya tathimini ya hasara ya jumla, kwa ajili ya kuangalia namna ya kutoa msaada wowote ule kwa waathirika  wa mafuriko hayo ili waweze kujikimu.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Malima amewataka Wanchi kuzingatia Sheria za Ujenzi  wa makazi yao ikiwemo kupata vibali vya Ujenzi ili kuondokana na madhara ya maafuriko kwa kuwa watafahamishwa na wataalam sehemu sahihi za ujenzi wa nyumba za makazi yao.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa  amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROAD) Eng. Lazack Kyamba kurudisha haraka mawasiliano ya Daraja la mto Mkondoa linalo unganisha Kilosa na Mikumi ili wananchi wa mji huo na wasafiri wengine wanaotumia njia hiyo ili waweza kuendelea na shughuli zao za kawaida.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amewashukuru Wananchi wa Wilaya hiyo kwa kuonesha ushirikiano wa kutosha kila yalipotokea mafuriko hivyo kuepusha madhara ya Kibinadamu ambayo yangeweza kutokea.

Sambamba na shukra hizo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa mitaro ya ya Barabara za Mjini Kilosa.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.