• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKULIMA WA MPUNGA KUNUFAIKA NA MRADI WA FTMA

Posted on: March 23rd, 2023

Wakulima wa zao la mpunga katika vijiji vya Kigugu, Mkindo na Iyombo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro wamenufaika na kilimo cha zao hilo chini ya programu ya Farm To Market Alliance (FTMA) ambayo imewawezesha kulima kwa tija zao hilo.

Hayo yamesemwa Machi 22 mwaka huu na Mkurugenzi wa Taasisi ya Farm Afrika Bi. Marry Batman wakati wa ziara yake iliyolenga kujionea hatua iliyofikiwa na wakulima hao tangu kuanzishwa kwa programu ya FTMA hapa nchini.

Bi. Marry amefafanua kuwa lengo la program ya FTMA ni kumsaidia mkulima kukutana na mashirika ambayo yanatoa ushauri juu ya kilimo bora cha Zap la mpunga kwa kuwapatia elimu, zana bora za kilimo, pamoja na kuwatafutia masoko ndani na nje ya nchi.

Aidha, amesema wamekuja kuangalia mafanikio, na changamoto ambazo wakulima hao wanazipata kupitia programu hiyo ambapo vikundi mbalimbali vinavyozalisha zao la mpunga kupitia kilimo cha umwagiliaji, hivyo wamefurahishwa kuona wakulima wamepata mafanikio makubwa japokuwa kuna changamoto ndogo ambazo zikifanyiwa kazi zitaisha kabisa.

"...tumekuja kuangalia wanafanyaje kwenye hii programu na tumeona shamba darasa ambalo wamepanda aina tano za mpunga na hivyo itawasaidia kuchagua mbegu bora ambayo wanaweza kuitumia kwa msimu ujao wa kilimo..." amesema Bi. Marry.

Akitoa shukrani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi huo kwa niaba ya wakulima wa Kijiji cha Mkindo Katibu wa Chama cha wakulima Bi. Khadija Rashid amesema kupitia mradi huo uzalishaji umeongezeka kwa sababu ya matumizi ya zana bora za kilimo ambazo wamezipata kupitia mradi huo.

Aidha, ameongeza kuwa mradi huo umewawezesha kupata soko la uhakika ambapo kampuni ya MW RICE MILLERS LTD ya Mkoani Morogoro inanunua mazao yao na kuwapatia wakulima hao mbegu bora zilizofanyiwa utafiti na TARI, DAWA na kupata elimu ya kilimo Chenye tija.

Hata hivyo, Katibu huyo amesema kupitia mradi huo umewawezesha kupata elimu ya  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kulima kilimo shadidi ambacho kina tumia maji kidongo na mbegu kidogo lakini mavuno yake ni mengi.

Kwa upande wake Bw. Seifu Rashidi Abdalah ambaye ni mkulima katika skimu hiyo amemuomba Mkurugenzi wa FTMA kuimarisha upatikanaji wa  masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi hivyo itawaongezea tija kwenye uzalishaji wa mpunga hii ni kutokana na kubadilika badilika kwa bei ya mpunga na mchele kwenye soko la dunia.

Mradi wa FTMA ulianzishwa kwa lengo la kumuwezesha mkulima kukuza kipato chake kwa kupata elimu, mbegu bora na zana za kisasa.

Mradi wa FTMA unafanya kazi katika nchi nne za Afrika ikiwemo Tanzania, Msumbiji, Rwanda na Kenya.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.