• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKULIMA WA MPUNGA KUNUFAIKA NA MRADI WA FTMA

Posted on: March 23rd, 2023

Wakulima wa zao la mpunga katika vijiji vya Kigugu, Mkindo na Iyombo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro wamenufaika na kilimo cha zao hilo chini ya programu ya Farm To Market Alliance (FTMA) ambayo imewawezesha kulima kwa tija zao hilo.

Hayo yamesemwa Machi 22 mwaka huu na Mkurugenzi wa Taasisi ya Farm Afrika Bi. Marry Batman wakati wa ziara yake iliyolenga kujionea hatua iliyofikiwa na wakulima hao tangu kuanzishwa kwa programu ya FTMA hapa nchini.

Bi. Marry amefafanua kuwa lengo la program ya FTMA ni kumsaidia mkulima kukutana na mashirika ambayo yanatoa ushauri juu ya kilimo bora cha Zap la mpunga kwa kuwapatia elimu, zana bora za kilimo, pamoja na kuwatafutia masoko ndani na nje ya nchi.

Aidha, amesema wamekuja kuangalia mafanikio, na changamoto ambazo wakulima hao wanazipata kupitia programu hiyo ambapo vikundi mbalimbali vinavyozalisha zao la mpunga kupitia kilimo cha umwagiliaji, hivyo wamefurahishwa kuona wakulima wamepata mafanikio makubwa japokuwa kuna changamoto ndogo ambazo zikifanyiwa kazi zitaisha kabisa.

"...tumekuja kuangalia wanafanyaje kwenye hii programu na tumeona shamba darasa ambalo wamepanda aina tano za mpunga na hivyo itawasaidia kuchagua mbegu bora ambayo wanaweza kuitumia kwa msimu ujao wa kilimo..." amesema Bi. Marry.

Akitoa shukrani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi huo kwa niaba ya wakulima wa Kijiji cha Mkindo Katibu wa Chama cha wakulima Bi. Khadija Rashid amesema kupitia mradi huo uzalishaji umeongezeka kwa sababu ya matumizi ya zana bora za kilimo ambazo wamezipata kupitia mradi huo.

Aidha, ameongeza kuwa mradi huo umewawezesha kupata soko la uhakika ambapo kampuni ya MW RICE MILLERS LTD ya Mkoani Morogoro inanunua mazao yao na kuwapatia wakulima hao mbegu bora zilizofanyiwa utafiti na TARI, DAWA na kupata elimu ya kilimo Chenye tija.

Hata hivyo, Katibu huyo amesema kupitia mradi huo umewawezesha kupata elimu ya  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kulima kilimo shadidi ambacho kina tumia maji kidongo na mbegu kidogo lakini mavuno yake ni mengi.

Kwa upande wake Bw. Seifu Rashidi Abdalah ambaye ni mkulima katika skimu hiyo amemuomba Mkurugenzi wa FTMA kuimarisha upatikanaji wa  masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi hivyo itawaongezea tija kwenye uzalishaji wa mpunga hii ni kutokana na kubadilika badilika kwa bei ya mpunga na mchele kwenye soko la dunia.

Mradi wa FTMA ulianzishwa kwa lengo la kumuwezesha mkulima kukuza kipato chake kwa kupata elimu, mbegu bora na zana za kisasa.

Mradi wa FTMA unafanya kazi katika nchi nne za Afrika ikiwemo Tanzania, Msumbiji, Rwanda na Kenya.

MWISHO.

Matangazo

  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro April 13, 2023
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • View All

Habari Mpya

  • RC Morogoro atembelea mabweni ya shule yaliyoteketea kwa moto, atoa maagizo

    June 05, 2023
  • RAS Morogoro awataka Viongozi waSerikali kujitathmini utekelezaji wa mkataba wa Lishe.

    June 03, 2023
  • RC MOROGORO AKUTANA NA WADAU WA MAENDELEO KUJADILI MUELEKEO WA MKOA.

    June 02, 2023
  • RC MALIMA AKABIDHIWA OFISI RASMI, AAHIDI KUWEKA MIKAKATI KUUENDELEZA MKOA HUO.

    June 01, 2023
  • View All

Video

Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.