• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAKULIMA WATAKIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA USHIRIKA.

Posted on: October 8th, 2024

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) amewataka wakulima wa Wilaya ya Gairo na wakulima wote hapa nchini kujiunga na vyama vya ushirika kwa ajili ya kuinua uchumi katika familia zao na kwa ajili ya maslahi mapana ya sekta ya kilimo.

Naibu Waziri Silinde amesema hayo Oktoba 8, Mwaka huu wakati akifungua maonesho ya Samia Kilimo Biashara Expo 2024 msimu wa tatu yaliyofanyika Wilayani Gairo yakiwa na lengo la kuongeza uelewa kwa wakulima ili kulima kilimo cha kisasa na cha kibiashara.

"... niombe na nitoe rai kwa wananchi wote wa Gairo kuendelea kujiunga na vyama vya ushirika na Watanzania wote katika maeneo yote nchini wajiunge na ushirika..." amesema Waziri.  

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema katika Wilaya ya Gairo kumekuwa na muitikio mkubwa ya wakulima kujiunga na vyama vya ushirika kwani mpaka sasa vyama vya ushirika 13 vimesajiliwa katika Wilaya hiyo, hivyo ameiagiza Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) kusajili vyama vingi Wilayani humo kwani amesema hiyo ni mojawapo ya kutatua changamoto ya masoko na pembejeo za kilimo.

Aidha, Naibu Waziri amewataka wakulima kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuwa mfumo huo unawasaidia wakulima kuuza mazao yao kwa bei elekezi na iliyopo kwenye masoko hivyo kuongeza kipato chao.

Katika hatua nyingine ameipongeza  Wizara ya Nishati kwa maonesho yao ya mfumo rafiki wa nishati safi ya kupikia yakiwemo majiko ya kupikia ikiwa ni kuunga mkono ajenda ya Mhe. Dkt. Samiaa Suluhu Hassan kwa maono ya kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo Gesi, umeme, mkaa mweupe na nyingine ili kuepuka uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.

Hata hivyo, Naibu Waziri huyo amewaagiza Wakuu wa Wilaya wote hapa nchini kuiga mfano wa Wilaya ya Gairo kuwa na maonesho ya Kilimo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima, kulima kisasa zaidi na kuwaletea tija.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ameleta mageuzi katika sekta ya kilimo kutokana na uhitaji wa wakulima kwani zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania hapa nchini wanategemea kilimo, hivyo mageuzi hayo yamelenga kuondoa umasikini ndani ya jamii inayotegemea kilimo na ufugaji.

Naye, Naibu Mrajisi (Uhamasishaji) wa TCDC Bi.Consolata Kiluma amesema Tume hiyo itahakikisha inasajili vyama vingi vya Ushirika na kuvisimamia na kutumisa hiyo kutoa wito kwa wakulima kujiunga na vyama hivyo kwani lengo la vyama hivyo ni kukuza uchumi kwa wananchi.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.