• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Morogoro watakiwa kubainisha maeneo hatarishi kukumbwa na kipindupindu.

Posted on: January 18th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kubainisha maeneo yenye uwezekano wa kuathiriwa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kuweka mikakati ya kuudhibiti mapema hivyo kunusuru maisha ya watu.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Januari 17 mwaka huu kwenye kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ngazi ya Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwa sasa hakuna mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ndani ya mkoa huo lakini Mkoa unaendelea kuchukua taadhari zote juu ya mlipuko wa ugonjwa huo huku akiwataka Wakurugenzi hao kushirikiana na wataalam wa afya kubainisha maeneo ambayo yako hatarini kupata ugonjwa huo hususan maeneo yenye mikusanyiko ya watu.

"...Pili nenda kaunde timu yako, nendeni mkaangalie maeneo ambayo yanaonekana kuwa ni hatarishi hayo ni maagizo yangu..." amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ametaja baadhi ya maeneo yanayoweza kuathirika na ugonjwa huo kwa haraka kuwa ni pamoja na Manispaa ya Morogoro, Kilosa, Mikumi, na Ifakara kutokana na maeneo hayo kuwa na mwingiliano wa watu wengi hivyo amewataka wakurugenzi wa Halmashauri hizo wakishirikiana na wakazi wa maeneo hayo kuchukua taadhari kwa kufanya usafi katika masoko, vyoo vya stendi na maeneo mengine.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio ameeleza kuwa hadi kufikia Januari 17 mwaka huu hakuna taarifa yoyote iliyoripotiwa katika vituo vya Afya juu ya kuwepo kwa ugonjwa huo. Aidha, ameongeza kuwa Mkoa umepokokea vifaa tiba kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa kipindupindu endapo kwa watabainika.

Nao Viongozi Dini akiwemo Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania (K.K.K.T) Dayosisi ya Morogoro Askofu Jacob Mameo amewashauri Wanasiasa kuacha kabisa tabia ya kuwakingia kifua wananchi wanaofanyabiashara katika maeneo yaliyokithiri kwa uchafu hasa pale Watendaji wa Serikali wanapowaondoa wafanyabiashara katika maeneo hayo.

Amesema lengo la watendami hao wa serikali daima huwa linakuwa jema la kunusuru vifo  vinavyoweza kutokana na mazingira hayo machafu, hivyo ni vema pande zote mbili zikawa na lengo moja la kutaka kuokoa maisha ya watu badala ya kuingiza siasa kwenye suala la maisha ya watu.

Kwa upande wake Mtaalam wa Epidemiolojia Mkoa wa Morogoro Dkt. Jonhas Masatu amebainisha njia za kujikinga dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu kuwa ni pamoja na usafi wa mazingira na usalama wa chakula, kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, kusafisha vyoo wa mara kwa mara pamoja na kudhibiti mifumo ya maji taka.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.