• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Walimu wakuu wekeni mazingira rafiki kwa walimu kushiriki MEWAKA - Dkt. Mutahabwa.

Posted on: July 4th, 2024

Kamishna wa Elimu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dkt. Lyabwene Mutahabwa amewataka walimu wakuu wote Nchini kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia walimu  kupata mafunzo endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA).

Dkt. Mutahabwa ametoa agizo hilo Julai 4, 2024 wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wakuu wa shule za Msingi na Sekondari na Maafisa mazingira katika usimamizi wa miradi ya maendeleo yaliyofanyika chuo cha Ualimu  cha Morogoro kilichopo Halmashauri ya Manispaa hiyo.

Dkt . Mutahabwa amesema, Serikali imeendelea kuboresha Sekta ya Elimu hivyo mafunzo hayo ya MEWAKA ni muhimu kwa walimu kuyapata yatakayojenga uwezo wa kutoa elimu bora kwa wanafunzi.

"....Nawaelekeza walimu wakuu kote nchini kwenda kuweka mazingira rafiki yatakayowavutia walimu kushiriki kikamilifu mafunzo ya MEWAKA..." Amesisitiza Dkt.Mutahabwa.

Aidha, kiongozi huyo amesema Serikali imekuwa na mafanikio makubwa katika kuboresha elimu msingi ikiwemo kuongezeka kwa uandikishaji wa wanafunzi katika ngazi mbalimbali, kuboreka mazingira ya kufundishia na kujifunzia, kuongezeka kwa wanafunzi wanaomudu stadi za kuandika, kusoma na kuhesabu na kuongezeka kwa ufaulu katika upimaji wa mitiani ya Taifa katika ngazi ya elimu ya msingi na sekondari.

Pia Dkt. Mutahabwa amewataka walimu kuimarisha usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji hususan darasa la awali kwa kuwa ndio msingi wa wanafunzi kumudu ( kusoma, kuandika  na kuhesabu - KKK ). Uimarishaji huo ametaka uende hata kwenye kuongeza ubunifu katika kutatua  changamoto za kujifunza ikiwa ni pamoja na matumizi ya zana na vifaa vilivyo boreshwa katika ufundishaji.

Katika hatua nyingine kiongozi huyo amewasisitiza walimu hao kuweka mifumo ya kuwalinda watoto dhidi ya unyanyasaji na ukatili kwa watoto ikiwemo kuundwa kwa vilabu vya wanafunzi ili waweze kujitambua, kujielewa na kujiamini na kushirikiana na jamii katika kubaini masuala ya ukatili na unyanyasaji kwa watoto.

"... Ulinzi na usalama wa mtoto uwe kipaumbele chetu.." amesisitiza kiongozi huyo.


Kwa upande wake Mratibu wa Program ya BOOST kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Ally Swalehe amesema program hiyo inaimarisha ufanisi wa ujifunzaji na ufundishaji, inaboresha elimu ya awali na msingi pia inatekeleza ujenzi wa miundombinu ambapo katika mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya shule 302 zimejengwa nchi nzima ambapo vyumba vya madarasa 7230, matundu ya vyoo 11297 na ukamilishaji wa vyumba vya madarasa 4770 vinaendelea kukamilishwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Maalum ya watu wazima amesema mafunzo hayo yana   lengo la  kuwajengea uwezo Maafisa mazingira na wakuu wa shule zinazopokea fedha za ujenzi wa miondombinu kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha usimamizi wa miundombinu na kusimamia manunuzi kwa kuzingatia mfumo wa NEST ili kuondoa changamoto ambazo zinajitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.