• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wamachinga’ Morogoro sasa kupatiwa mikopo.

Posted on: October 20th, 2021

‘Wamachinga’ Morogoro sasa kupatiwa mikopo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amemuagiza Mwenyekiti wa Wafanya biashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga Mkoani humo Bw. Faustine France kuunda vikundi vya wafanya biashara hao na kuwasilisha maombi ya mikopo yao Ofisi za Halmashauri za Mkoa huo kwa ajili ya kupewa mikopo ya kukuza biashara zao.

Shigela ametoa agizo hilo Oktoba 19 mwaka huu alipokuwa anakagua maeneo yaliyokuwa yanatumiwa  na wamachinga yasiyo rasmi kwa ajili ya kufanya biashara zao ili kujiridhisha kama wameondoka na kuhamia kwenye vibanda walivyojengewa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando katika Soko Kuu la Chief Kingalu kwa Kushirikiana na Wahe. Madiwani wa Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (kushoto) akikagua maeneo ambayo yalikuwa yanatumiwa na wamachinga kufanya biashara zao, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando.

Amesema Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameelekeza Halmashauri zote nchini kutenga pesa kwa ajili ya kuwawezesha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu hivyo Mwenyekiti wa machinga aunde vikundi ili wamachinga waweze kunufaika na pesa hiyo kwa kujiunga katika vikundi ili wakopeshwe na kukuza mitaji yao.

‘’….Wamachinga kwa sasa wanajulikana walipo wana namba na  anuani, nielekeze Mwenyekiti, unda vikundi peleka kwenye Halmashauri zote, omba kiasi cha fedha unazozihitaji kwa ajili ya vikundi vyako….’’ aliagiza Shigela.

Aidha, amesema mara baada ya Mwenyekiti kuwasilisha maombi ya fedha hizo katika Halmashauri za Mkoa huo atahakikisha anafuatilia mikopo hiyo ili itoke haraka na iweze kuvisaidia vikundi hivyo katika kujikwamua kimaisha.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela  (wa tatu kushoto) akizungumza na wafanyabiashara ya samaki ambao walikuwa wamebaki katika sehemu ambayo siyo rasmi kufanyia biashara hiyo.

Sambamnba na hayo, Shigela amesema katika maeneno ambayo hayajakamilika rasmi kwa ajili ya kutumika na wamachinga hao, tayari Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro na Mkuu wa Wilaya hiyo wameshakamilisha andiko hivyo wakimkadhi ataliwasilisha TAMISEMI ili watoe fedha kwa ajili ya kukamilisha maeneo  ambayo hayajakamilika.

Hata hivyo amewataka baadhi ya wamachinga ambao hawajatoka katika maeneo ambayo yamekatazwa kufanyia biashara kutii sheria bila shuruti kwani muda waliokuwa wamepewa umekwishapita na Serikali imeweka utaratibu huo kwa nia njema ya kuwajengea mfumo mzuri wamachinga  kukaa katika maeneo ambayo yameainishwa na kurasimishwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando amempongeza Mkuu wa Mkoa huo kwa ushirikiano wa dhati anaoutoa kwa wamachinga katika kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya biashara zao bila kutumia nguvu katika kutatua changamoto za wamachinga.

Aidha, Msando amesema andiko la kuwasilisha maeneo ambayo hayajakamilika watahakikisha wanalifanyia kazi na kuwasilisha mapema katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili pesa ambazo zimetengwa kwa ajili ya vikundi ziweze kuwanufaisha wamachinga kwa sababu kuna wamachinga vijana, wenye ulemavu na  kuna wamachinga kina mama ambao kwa ujumla wana sifa za kupata mkopo huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (kushoto) akiwa nje ya Soko la Chifu Kingalu akiangalia namna ambavyo atapanua miundombinu ya kufika ndani ya soko hilo.

Naye Mwenyekiti wa Wamachinga Mkoa wa Morogoro Faustine France amewataka wafanyabiashara wote wa mtaa wa Islam, Shani na maeneo mengine ndani ya Manispaa ya Morogoro kutofanya biashara katika maeneo hayo wakisubiria maelekezo ya Serikali ya kuwapeleka maeneo watakayofanyia biashara zao.

Katika hatua nyingine  France maarufa kama White amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuunda vikundi hivyo ili kila machinga mwenye uhitaji aweze kupatiwa mkopo kwa ajili ya kukuza biashara yake.

MWISHO.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.