• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANACHI KIJIJI CHA WAMI LUHINDO WAHAMASIKA KUJENGA SHULE, WAOMBA SIKU YA HARAMBEE IPANGWE KARIBU.

Posted on: January 17th, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Wami Luhindo kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro wamehamasika kutoa michango yao wa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi ili kuwaokoa watoto wao dhidi ya wanyama wakali na kusafiri umbali wa zaidi ya kilometa 8 kufuata kusoma shule ya Msingi Mawasiliano ambayo iko eneo la Makunganya.

Hayo yamebainika Januari 16 mwaka huu wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare Wilayani mvomero ambapo alifanya mkutano wa hadhara wa kijiji eneo la Wami Vijana maarufu kama Maji chumvi kwa ajili ya kutatua mgogoro wa Ardhi ambapo baadhi ya wananchi wengi wao inasemekana ni wa kutoka katika Manispaa ya Morogoro ndio waliovamia eneo hilo la wawekezaji na kusababisha mgogoro huo.


Baada ya kuhitimisha changamoto ya mgogoro huo wa ardhi na kuonekana asilimia kubwa ya wakazi wake wameingia kimakosa kwa kurubuniwa na baadhi ya wenyeviti wa Vitongoji katika maeneo hayo ya wawekezaji wanaojulikana kama General Mbowe na Balozi Namfua ndipo wananchi hao wakaibuka na kero ya kutaka kujua ni lini ujenzi wa shule yao utakamilika.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Kata ya Dakawa Haji Luvanga, ujenzi huo wa shule unaohusisha madarasa manne na Ofisi moja ya mwalimu ulianza mwaka 2013 na haukukamilika kwa wakati kutokana na changamoto ya kujengwa ndani ya eneo la wawekezaji hao.

Hata hivyo Mtendaji Haji Luvanga amesema kwa jitihada za Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Albinus Mgonya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Njama Hassan Njama wamefanikiwa kutatua changamoto hiyo na tayari kijiji kimepokea kibali cha kuendelea na ujenzi wa shule hiyo.

Baada ya Taarifa hiyo wananchi walionesha kuahamasika na kumtaka aanzishe mchango kwa ajili ya ujenzi huo na wao wako tayari kuchangia ili shule hiyo iweze kukamilika haraka hivyo kunusuru watoto wao.

Akihitimisha changamoto hiyo ya migogoro ya Ardhi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amewataka wananchi wa kijiji cha Wami Luhindo kufuata sheria katika kupata ardhi huku akiwanyooshea kidole wawekezaji kuwa miongoni mwao ni chanzo cha migogoro ya ardhi Mkoani Morogoro kwa kubaki na maeneo yao kwa muda mrefu bila kuyaendeleza na kusababisha migogoro ya mara kwa mara.

Kwa sababu hiyo amesema atamwomba Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Waziri wa Ardhi na Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kuyafuta umiliki mashamba yote yasiyoendelezwa kwa wakati.

Kuhusu shule, Loata Sanare amesema Elimu ndiyo itawaletea maendeleo wananchi wa Luhindo na hana shaka kijiji hicho watatekeleza kwa ufanisi kwa vile wameonesha shauku katika kujenga shule yao, na kwamba kwa kufanya hivyo siku moja kiongozi mkubwa atatoka katika shule yao.

“ msisubiri mtu mwingine akuleteeni maendeleo, tujitolee…shule hiyo ndiyo itatusaidia, shule hiyo ndio atatoka kiongozi mwingine si dhambi miaka ijayo Mkuu wa Mkoa akatoka mtoto mmoja aliyesoma maji chumvi…” alisema Loata Sanare.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Albinus Mgonya alimjulisha Mkuu wa Mkoa kuwa siku ya harambee ya kuchangia ujenzi wa shule hiyo itakuwa Januari 20 mwaka huu na kutaka wananchi wote kujitokeza huku akiongelea kuhusu wananchi walioharibiwa mazao yao na wanyama pori na kuhitaji kifuta jasho ambapo jumla ya ekari 11,000 za mashamba ziliharibiwa.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.