• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANAFUNZI 100 WAFUZU.

Posted on: May 30th, 2021

Jumla ya Wanafunzi 100 kati ya 650 na walimu 15 kati ya 100  kutoka katika Wilaya tisa za Mkoa wa Morogoro wamefuzu kuendelea na  mashindano ya UMITASHUMTA ambapo wataunda timu moja ya kuuwakilisha Mkoa wa Morogoro kitaifa.

Hayo yamebainishwa Juni Mosi, 2021 na Afisa Michezo wa Mkoa wa Morogoro Bi. Grace Njau wakati wa kufunga Michezo ya Umitashumta iliyofanyika katika Shule ya Kilimo ya Kilosa iliyopo Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.

‘’…Ni wanafunzi 100 tu kati ya 650 ambao wamefuzu na walimu karibia 15 tu ambao wataenda kuuwakilisha Mkoa wa Morogoro kitaifa kuanzia Juni 6 hadi 19 mwaka huu Mkoani Mtwara…’’ Ameme Grace.

Aidha, Bi. Grace amesema adhima ya Serikali ya kuandaa mashindano ya Umitashumta kila mwaka ni kuandaa timu itakayo iwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia (World Cup) hivyo Mkoa unapambana kuhakikisha washindi katika mashindano haya wanakuza vipaji vyao na kuviendeleza.


Pia, Bi. Grace amesema Mkoa wa Morogoro ni Miongoni mwa Mikoa bora inayozalisha wanamichezo bora kitaifa na kimataifa  hususan kwenye soka la wanaume wakiwemo Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, Jonas Mkude, Kibwana Shomari, Hassan Kessy na Kelvin John ambaye anacheza soka la kulipwa nchini Ulaya.

Katika hatua nyingine, Bi. Grace amebainisha changamoto mbalimbali walizokumbana nazo wakati wa mashindano hayo ni baadhi ya walimu kutofundisha michezo kikamilifu mashuleni, ukosefu wa walimu waamuzi wa mpira, ukosefu wa madaktari waliosomea tiba maalumu kwa wachezaji na michango ya Omitashumta kutokamilishwa kwa wakati.

Kwa upande wake Mgeni rasmi wa mashindano hayo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Francis Kaunda, amewataka Walimu waliochaguliwa kuongozana na timu ya Mkoa kuhakikisha wanarudi na ushindi na kuwataka walimu ambao wamekuwa wakipewa timu kisha kurudi bila ushindi wabadilishwe ili kuongeza ushindani.

Sambamba na hayo, Ndg. Kaunda ametoa pongezi kwa wanamichezo walioshinda katika michezo mbalimbali na kuwataka wale ambao hawakufudhu kuunda timu ya Mkoa kuongeza bidii ili mwaka ujao waweze kufanya vizuri Zaidi.

‘’Napenda kuwapongeza wanamichezo wote walioshinda katika michezo mbalimbali na asiyekubali kushindwa si mshindani. Ila kama umeshindwa leo haimaanishi kwamba wewe hujui michezo, unajua ndio maana umefika ngazi ya Mkoa, hivyo uongeze bidii ili mwaka ujao ufanye vizuri’’ Amesema Kaunda.

Mashindano ya Omitashumta Mkoani Morogoro yalianza Mei 30, 2021 baada ya kufunguliwa rasmi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kilosa ambayo yalihusisha takribani watu 789 wakiwmo walimu na wanamichezo.

Mashindano hayo yalihusisha mpira wa miguu, pete, kengele, nyavu, wavu, mikono, usafi na nidhamu, kwaya na riadha.

Kaulimbiu ya Mashindano hayo ilikuwa ni ‘’ MCHEZO, SANAA  KWA MAENDELEO YA VIWANDA’’


 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.