• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza watakiwa kuripoti kesho Januari 16,2023

Posted on: January 15th, 2023

WANAFUNZI WALIOFANYA MTIHANI WA MARUDIO WATAKIWA KURIPOTI SHULENI KESHO JANUARI 16,2023.

Wanafunzi waliofanya mtihani wa Marudio wa darasa la saba 2022 na kuchaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa kesho Januari 16 Mwaka huu bila kuweka kikwazo chochote ili kwenda pamoja na wanafunzi wenzao kimasomo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe

Taarifa hiyo imetolewa leo Januari 15 mwaka huu na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe mbele ya waandishi wa Habari katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Akifafanua zaidi Prof. Shemdoe amesema wanafunzi hao wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2023 baada ya kurudia mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba uliofanyika tarehe 21 hadi 22 Disemba 2022.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo amewaagiza wazazi na walezi wote wa wananfunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika mtihani huo wa marudio kuwapeleka shule watoto wao shuleni bila kuweka kisingizio chochote.

Baadhi ya Viongozi waandamizi ngazi ya Mkoa wakati Katibu Mkuu TAMISEMI akitoa taarifa hiyo. kushoto kwa Katibu Mkuu ni Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa na kulia kwake ni Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Elimu (Afisa Elimu Mkoa) Bi. Germana Mung'aho

akitoa taarifa hiyo Prof. Shemdoe amesema Ofisi ya Rais – TAMISEMI imepokea matokeo ya mtihani huo hivi karibuni kutoka Baraza la mitihani la Taifa ambapo jumla ya wanafunzi 2,096 wakiwemo wavulana ni 1,073 na wasichana ni 1,023 sawa na asilimia 96.15 ya watahiniwa waliofanya mtihani wamepata sifa ya kuchaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza katika Shule za Sekondari za Serikali.

Aidha, Katibu Mkuu huyo ameongeza kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na Kamati za Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Mikoa husika imekamilisha zoezi la kuwapangia Shule wanafunzi wote 2,096 katika Shule mbalimbali za Sekondari na Maandalizi ya kuwapokea wanafunzi hao yamekamilika hivyo wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa.

“Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika mikoa husika imekamilika zoezi la kuwapangia Shule wanafunzi wote 2,096 katika Shule mbalimbali za Sekondari. Maandalizi ya kuwapokea wanafunzi hao yamekamilika na wanataarifiwa kuripoti katika Shule walizopangiwa siku ya Jumatatu tarehe 16 Januari 2023 ili kuanza masomo.” amesema Prof. Shemdoe.

Sambamba na hilo Prof. Shemdoe ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha kuwa wanawaandikisha watoto wao shule za msingi ili waweze kuanza masomo ya awali na darasa la kwanza.

Awali, Baraza la Mitihani la Tanzania lilitoa taarifa ya Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Marudio kwa wanafunzi wa Darasa la Saba mwaka 2022 ambapo jumla ya wanafunzi 2,194 wakiwemo wavulana 1,117 na wasichana 1,077 walitakiwa kufanya mtihani huo kuanzia Disemba 21 – 22, 2022 kwa sababu matokeo yao yalifutwa kwa mujibu wa kifungu 30(2)(b) cha Kanuni za Mitihani 2016 kikisomwa pamoja na kifungu cha 5(2)(i) na (j) cha sheria cha Baraza la Mitihani Sura ya 107.Jumla ya wanafunzi 2,180 wakiwemo wavulana 1,112 na wasichana 1,068 sawa na asilimia 99.36 walifanya mtihani huo wa marudio.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.