• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANANCHI 6000 GAIRO WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Posted on: May 25th, 2022

WATU 6000 WILAYANI VIJIJI VYA IYOGWE NA KINYOLISI WILAYANI GAIRO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Wananchi zaidi ya 6000 wa kijiji cha Iyogwe Wilayani Gairo Mkoani Morogoro wako mbioni kupata maji safi na Salama baada ya Serikali ya awamu ya sita kupeleka zaidi ya Tsh. 500Mil. Kwa ajili ya kuwaondolea wananchi wa kijiji hicho kero hiyo ya Maji.


Hayo yamebainika wakati wa ziara ya siku mbili ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Wilayani humo ambapo pamoja na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo, ametembelea mradi wa Maji wa utakaogharimu Tsh. 513Mil. Ambapo utanufaisha wananchi 6000 wa vijiji viwili vya Iyogwe na Kinyolisi.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Kinyolisi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (hayupo pichani) alipofanya ziara kijijini hapo Mei, 25 mwaka huu


Akiwa katika kijiji cha Kinyolisi ambapo mradi huo unatekelezwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela pamoja na kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazanaia amemuagiza Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa Wilaya ya Gairo Paascal Jeremia kuhakikisha mradi huo unakamilika mwezi juni mwaka huu ili kuwaondolea wananchi kero ya maji waliyokuwa wanaipata.



“Meneja wa RUWASA nikuagize nataka tarehe therathini uje ujaribu vituo vyote kama vinatoa maji kwenye kituo hiki ili wananchi wetu wanaohangaika kupata maji waweze kupata maji” amesema Shigela.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza wananchi wa Kata ya Iyogwe kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 23 Mwaka huu ili serikali kupata takwimu sahihi zitakazosaidia utoaji wa huduma mbalimbali za Maendeleo ya wananchi  kwa uhakika zaidi.


Mkuu wa Wilaya ya Gairo Omary Makame akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuongea na wananchi wa Kijiji cha Iyogwe alipofanya ziaya Wilayani humo

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabiri Omary Makame amebainisha kuwa kukamilika kwa mradi wa maji wa Kinyolisi kutawasaidia wananchi wa eneo kujihusisha na masuala ya maendeleo zaidi badala ya kutafuta maji kwani kwa sasa wananchi hao wanatumia maji ya visima tena kwa hupanga foleni hivyo kupoteza muda mwingi.






Mhe. Recho Nyangasi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wialya ya Gairo wakati wa mkutano wa hadhara Kijiji cha Iyogwe  wakati ziara ya Mkuu wa Mkoa

Naye diwani wa kata ya Chakwale Mhe. Ramadhani Kimwaga pamoja na kuishukuru Serikali kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo, ameeleza changamoto zinazoikabili Kata hiyo kuwa ni pamoja na changamoto ya miundombinu ya barabara yakiwemo madaraja.




Kwa upande wake Steven Mchongi ambaye ni mwenyekiti wa Shule ya msingi Kilimani amemuomba Mkuu wa Mkoa kutatua  changamoto ya madawati inayoikabilia shule yake ambayo wanafunzi zaidi ya 304 hawana madawati ya kukalia.



MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.