• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi Dumila wataka viongozi wachukuliwe hatua.

Posted on: October 6th, 2021

Wananchi wa Kata ya Dumila Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wameiomba Serikali kuwachukulia hatua viongozi waliohusika na upotevu wa pesa zaidi ya Shilingi Mil. 800 zilizotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji.

Wananchi wametoa ombi hilo Oktoba 5 mwaka huu mbele ya Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela alipofanya  ziara ya siku moja Wilayani Kilosa kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi kupitia mikutano ya hadhara.

Wananchi wa kata ya Dumila wakiwa katika mkutano wa hadhara wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akitoa maelekezo juu ya kero zao.

Akizungumza katika Mkutano huo mwananchi Issa Mkumbuko amesema Novemba  2011 Serikali ilipeleka shilingi Mil. 800 zilizofadhiliwa na Benki ya dunia kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji katika kata ya Dumila lakini pesa hizo hazikutumika kufanya miundombinu hiyo.

‘’….Milioni 800 zilizotolewa na World Bank zimepotea kama ice cream motoni  hazijulikani zilipo, hizo milioni zimepotea hazijafanya kazi hadi sasa’’…. amesema Mkumbuko.

Katika hatua nyingine mwananchi huyo amesema mbali na Serikali kutoa pesa hizo tayari wananchi walikuwa wamechanga jumla ya shilingi Mil. 18 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo ambazo nazo hazijulikani matumizi yake.

Mmoja kati ya wananchi waliohudhuria mkutano huo akitoa kero kwa niaba ya wananchi wa kata ya Dumila.

Naye Joseph Kosmas  amebainisha changamoto nyingine inayowakabili wananchi wa Dumila kuhusu changamoto ya maji ni kutokuwepo kwa chombo cha kutoa huduma ya maji ambacho kingesaidia kutatua kero za maji na kurahisisha upatikanaji wa maji katika kata hiyo.

Amesema Uongozi wa uliopo wa chombo hicho imeundwa na watu kwa wachache kwa maslahi yao binafsi na hakijishughulishi na lolote katika kutengeneza miundombinu ya maji lakini pia jumuiya hiyo inajiendesha yenyewe bila wataalam wala mwakilishi kutoka kwa wananchi.

Baada ya kutolewa kero hizo za wananchi Mkuu wa Mkoa Martine Shigela  amefikia uamuzi wa kuvunja Uongozi wa chombo hicho cha kutoa huduma ya maji kilichokuwepo na kumuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga kwa kushirikiana na Mhandisi wa maji kutoka RUWASA Wilaya hiyo Joshi Chum kuitisha mkutano kwa ajili ya kuunda jumuiya mpya ya maji ambayo itaundwa kwa mujibu wa sheria na sifa zinazotambulika kwa lengo la kusimamia miundombinu ya maji.

Aidha, Shigela amesema mara baada ya kuundwa kwa chombo hicho lazima kiwajibika kwa wananchi kwa kuwafikishia huduma ya maji hususan katika vijiji ambavyo hadi sasa vinakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji.

Katika hatua nyingine Shigela amesema kutokana na uhitaji mkubwa wa maji katika Kata ya Dumila bado ameelekeza visima vya maji vinavyomilikiwa na Bw. Ndunda kuendelea kutoa huduma ya maji kwa wananchi bila kuzuiwa na mtu yoyote.

‘’Kwa hiyo Bw. Ndunda kama una pesa yako umehifadhi benki Milioni 200 kazichukue nenda sehemu yoyote ambayo unadhani wananchi wanahitaji maji wapelekee’’ ameagiza Shigela.

Akijibu tuhuma za upotevu wa fedha zinazodaiwa kupotea na kutumika ovyo ambazo zilitolewa na World Bank kupitia Serikali ya Tanznaia na zile zilizochangwa na wananchi, Mhandisi wa maji Wilaya ya Kilosa Joshi Chum amekiri kuletwa fedha hizo na kwamba zilitumika katika ujenzi wa miundombinu iliyopo kwa sasa ikiwa ni pamoja na kujenga visima viwili.

Aidha fedha hizo zilijenga tenki la maji la lita 300,000, zilinunua mambomba yaliyolazwa umbali wa Km 28, kujenga vituo 56 vya maji, kununua pampu ya umeme na kujenga nyumba ya kuhifadhia pampu hizo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga akizungumza na wananchi wa kata ya Dumila.

Kuhusu fedha zilizochangwa na wananchi Mhandisi Chum amesema anachokijua ni shilingi Mil. 9 zilitumika kununulia mita ya Umeme huku nyingine zikitumika kwa ajili ya uendeshaji wa chombo hicho kutoa huduma ya maji huku akisema kiasi kingine inaonesha kweli matumizi yake hayakuwa kwenye utatratibu na  suala hilo linafanyiwa kazi ili kuwachukulia hatua za kisheria watakaobainika kuhusika nazo.

Pamoja na majibu hayo,  Mhandisi Chum amekiri kupokea maagizo ya Mkuu wa Mkoa na kwamba anaendelea kuyafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuratibu upya uundwaji wa chombo cha kutoa huduma ya maji katika kata ya Dumila.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ametembelea Kata tatu za Mtumbatu na Dumila ambako alifanya mikutano ya hadhara na kutatua kero za wananchi pamoja na kukagua ujenzi wa daraja la Kiegea ambalo hadi sasa limefikia asilimia 90 ya ujenzi wake.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.