• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi Kilosa Waipongeza Serikali

Posted on: July 28th, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Chanzuru wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wameipongeza serikali kwa kuingilia kati mgogoro wa shamba lenye jumla ya Ekari 1598 uliokuwepo baina yao na mwekezaji Mihanga  Leizer  ambao umedumu kwa zaidi ya miaka 15 bila kutatuliwa.

Hatua ya kuipongeza Serikali  inakuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela kufika Kijijini hapo Julai 26 mwaka huu  na kueleza msimamo wa Serikali juu ya mgogoro wa shamba hilo kutoka kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Shigela amesema, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa maelekezo kuwa shamba hilo lirudishwe kwa wananchi kwa ajili ya kulitumia kufanya shughuli zao za kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na kilimo.

Kutokana na maelekezo hayo, Mkuu wa Mkoa huyo amempiga marufuku Mwekezaji Leizer kufanya shuguli yoyote ya kilimo ikiwa ni pamoja na kutovuna mazao ya wananchi aliyoyakuta huku akimtaka kutii maelekezo aliyopewa ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza.

‘’Ukitaka kuchukua ardhi na ukakuta  kuna maendelezo ambayo yamefanyika  ni lazima kulipa fidia kwa maendeleo yaliyofanyika, hivyo kuanzia leo ni marufuku kwa ndugu Laizer kuvuna mazao ambayo aliyakuta kwenye shamba hilo’’amesema Shigela.

Licha ya kumpiga marufuku mwekezaji huyo kuvuna mazao ya wananchi  aliyakuta katika shamba hilo, Shigela amemruhusu kuvuna mazao ambayo alipanda mwenyewe katika shamba hilo huku Serikali ikitafuta namna nzuri ya kutatua mgogoro huo.

Sambamba na hayo, Shigela amesema  Serikali itatambua pesa ambazo Mwekezaji huyo amezitumia katika shamba hilo lakini pia Serikali itatatambua na kuthamini wananchi zaidi ya 4000 waliopo katika kata ya Chanzulu wanaotumia hekari zaidi ya 1200 kwenye shamba hilo lenye hekari 1500

Kwa upande wake Kamishina wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Morogoro Frank Mizikuntwe amesema shamba hilo lilifutwa mwaka 2017 na mwaka 2018 likafanyiwa mpango wa matumizi bora ya Ardhi.

 Aidha, Mizikuntwe amesema  kwa mujibu wa maelekezo ya Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa alielekeza sehemu ya shamba hilo ambayo haifanyiwi matumizi yoyote ya kibinadamu apewe  mwekezaji huyo na sehemu ambayo wananchi wanatumia kwa makazi, mazao ya muda mrefu na muda mfupi wananchi hao waiendeleze kwa shughuli hizo.

Kwa upande wake mwekezaji Mihanga Laizer, amesema shamba hilo alilinunua kwa shilingi Mil. 90 na kukabidhiwa nyaraka zote za msingi kwa kufuata sheria zote za ununuzi wa ardhi zilizoendeshwa na wanasheria wa mahakama ya Wilaya ya  Kilosa Mkoani humo.

Mihanga amesema baada ya kununua shamba hilo aliandika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilosa kuomba kuainishiwa mipaka ya shamba hilo ambapo wataalam kutoka Wilayani Kilosa walifika shambani hapo na kumuwekea mipaka kwenye shamba lake.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho cha chanzulu akiwemo Shabani Shomvi wamempongeza Mkuu wa Mkoa Martine Shigela kwa kutatua Mgogoro huo uliodumu kwa kipindi kirefu  na kumuomba afike katika vijiji vingine kutatua migogoro hiyo ya Ardhi kikiwemo kijiji cha Ilonga.

 MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.