• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi Malinyi watakiwa kuchangia gharama ndogo za maji.

Posted on: January 19th, 2022

Mhandisi Mahundi awataka wananchi Malinyi kuchangia maji.

Naibu Waziri, Wizara ya maji Mhandisi MarryPrisca Mahundi amewataka wananchi Wilayani Malinyi kuendelea kuchangia gharama ndogo  za maji zinazotozwa na mamlaka husika ili kuendelea kupata huduma ya maji safi na salama.


Naibu Waziri amesema hayo Januari 17 mwaka huu wakati wa ziara yake Mkoani Morogoro na kukutana na wananchi wa Wilaya hiyo ambapo alitembelea miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa katika Wilaya hiyo kupitia Wakala wa Usambazaji wa Maji safi na Usafi wa Mazingira-RUWASA.


Naibu Waziri amesema kuwa miradi hiyo inatekelezwa kupitia fedha  za UVIKO 19 ambapo Wilaya ya Malinyi imepokea kiasi cha shilingi milioni 641 zilizotolewa na Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan, fedha hizo zitasaidia kutekeleza mradi mkubwa wa maji ambao utapeleka maji katika Kata za Changani, Itete njiwa pamoja na uchimbaji wa visima 14 mradi ambao utatekelezwa na wakandarasi watano.

“………. sisi tunaotumia tunachangishwa hatuuziwi maji, uongo? ninawasihi kuendelea kuchangia gharama ndogo za maji ambazo mnapangiana kulingana na mazingira yenu…….” alisisitiza Waziri.

Aidha, Mhandisi Mahundi amesema kuwa  lengo la Wizara sio kuwauzia maji wananchi wake isipokuwa wananchi wanapaswa kuchangia gharama za uendeshaji wa miradi ya maji kupitia michango hiyo wanayochangishwa ili kununulia madawa ya kutibu maji Pamoja na kununua umeme utakaotumika kusukuma hayo maji.

Sambamba na hilo Naibu Waziri amefafanua kuwa mradi huo wa uchimbaji wa visima 14 vya maji utatoa ajira kwa wakazi wa Wilaya hiyo pamoja na kutatua changamoto ya maji kwa wakazi wa eneo la mradi hivyo wananchi waendelee kutunza miundo mbinu ya maji.

Akitoa shukrani zake kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Mbunge wa Jimbo la Mlinyi Antipass Mgungusi amesifu kasi hiyo ya utendaji kazi wa Rais Samia na Serikali yake ya awamu ya sita ya kuhakikisha kuwa wananchi wake wanaondokana na changamoto ya maji na changamoto zingine kama vile umeme barabara na kwamba kupitia kasi hiyo mradi huo wa maji anaamini utakamilika kabla ya awamu ya pili ya uongozi wa Rais Samia.

Kwa upande wao wananchi wa Kitongoji cha  Makugila A, katika  Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Bi. Asha kwa niaba ya wananchi wenzake ameeleza adha waliyokuwa wanaipata na kwamba kutokana na ukame,  ulipelekea wao kutumia maji machafu yenye tope  hali ambayo ilipelekea kuugua homa ya matumbo Pamoja na kuhara.


Hata hivyo wananchi hao wanaishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya  dhati ya kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwasogezea huduma za maji safi na salama katika maeneo yao.


Wilaya ya Malinyi inavituo 643 vinavyotoa  huduma ya Maji Kati ya 703 vilivyopo. Takribani fedha Bilioni 3  Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 zimetengwa Kwa ajili ya kutatua changamoto ya Maji katika Wilaya hiyo.

Kwa sasa Hali ya upatikanaji wa Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi umefikia asilimia 70 ambapo zaidi ya wakazi 1400 wanapata huduma hiyo huku asilimia hiyo ikiwa nyuma ya lengo la Serikali kupitia Wizara ya Maji ya kuhakikisha kuwa upatikanaji wa Maji unafikia asilimia 85 vijijini na 95 mjini.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.