• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANANCHI MOROGORO WATAKIWA KUJITOKEZA KUPATA CHANJO YA UVIKO 19

Posted on: November 20th, 2022

Wananchi Mkoani Morogoro watakiwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata chanjo ya UVIKO 19 katika vituo vyote vya afya vinavyotoa huduma ya chanjo ili wawe salama na kuwakinga wengine dhidi ya ugonjwa huo hatari.

Wito huo umetolewa Novemba 19 mwaka huu na Dkt. Florian Tinuga Meneja wa Mpango wa Taifa wa Chanjo kutoka Wizara ya Afya wakati wa uzinduzi wa Awamu ya pili ya chanjo ya UVIKO -19 Mkoani Morogoro uliofanyika katika viwanja vya Jamhuri, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Dkt. Florian Tinuga amesema Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa ambayo imekuwa na mwitikio hafifu wa chanjo hiyo ambapo kwa sasa wananchi walio chanja ni asilimia 66.2 ukilinganisha na lengo la Taifa la asilimia 80.

Wahudumu wa Afya ambao wameandaliwa kutoa huduma ya chanjo ya Uviko - 19 kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro.

Aidha, Dkt. Florian Tinuga amesema ili Mkoa huo ufikie lengo hilo ifikapo Disemba mwaka huu uhamasishaji na utoaji wa elimu kwa wananchi unatakiwa kuendelea katika maeneo yote ndani ya mkoa Pamoja na kusogeza huduma hiyo ya chanjo karibu na wananchi.

Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua taadhari ya ugonjwa huo kwa kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya kwa kuwa ugonjwa bado ni tishio uliwenguni.

Meneja wa Mpango wa chanjo Taifa Dkt. Florian Tinuga (kushoto), Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa (katikati), na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio pamoja na Mwakilishi wa Wizara ya Afya wakishuhudia uzinduzi wa chanjo katika Mkoa huo.

Sambamba na hilo, Gerson Msigwa amewataka watanzania kuchukua taadhari ya ugonjwa wa Ebola ambao upo katika nchi Jirani za Uganda na Kongo, pia amewataka kutoa taarifa kwa wataalamu wa Afya pindi wanapoona viashiria vya ugonjwa wa Ebola.

Aidha, Gerson Msigwa amesema Serikali imechukua taadhari kwenye mipaka yote ya nchi na katika viwanja vya ndege vinavyopokea wageni kutoka nje ya nchi ili kubaini watu wenye viashiria vya ugonjwa huo tishio kwa sasa.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Albert Msando kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameishukuru Wizara ya Afya kwa kuzindua mpango wa chanjo ya Uviko 19 katika mkoa huo na kusema kuwa wananchi wapo tayari kwa zoezi la uchanjaji.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Albert Msando akihamasisha wananchi kupata chanjo ya Uviko - 19 katika Mkoa huo.

Aidha, Mhe. Albert Msando amewahakikishia wakazi wa mkoa huo kuwa chanjo hizo ni salama na hazina madhara yoyote kwa afya zao na kuwataka kupuuzia maneno ya upotoshaji yanayozushwa na baadhi ya watu wasio na mapenzi mema na nchi yetu au wasio na uelewa wa kitaalam juu ya chanjo hizo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa ameziagiza Halmashauri za Mkoa wa Morogoro kuhakikisha zinatoa elimu kwa wananchi wake ili wahamasike kuchanja Pamoja na kuwasogezea huduma hizo za chanjo karibu maeneo wanayoishi.

Wananchi wa Mkoa wa Morogoro wakishuhudia uzinduzi wa chanjo ya Uviko - 19 katika Mkoa huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.