• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi wa Chanzuru wafurahia uamuzi wa Waziri Mkuu

Posted on: September 9th, 2021

 

Wananchi wa Kijiji cha Chanzuru Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wamefurahishwa na uamuzi wa Serikali uliotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim majaliwa (MB) wa kufuta shamba la Mwekezaji Laizer Mihanga na kugiza shamba hilo kupewa wananchi wa Kijiji hicho kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Taarifa ya kufutwa shamba hilo lenye Ekari 1598 uliwasilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Septemba 8, mwaka huu alipofanya ziara Wilayani Kilosa kwa lengo la kuwasilisha uamuzi huo wa Serikali uliotolewa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

Shigela amesema amefanya ziara hiyo Wilayani humo kutekeleza agizo la Waziri Mkuu kufuta shamba hilo la Mkonge la Chanzuru ambalo awali lilikuwa linamilikiwa na Mwekezaji Mzawa Laizer Mihanga na kwamba kwa sasa Serikali imeamua shamba hilo wapewe wananchi kwa ajili ya shughuli za kilimo.

Shigela amesema maelekezo ya Mhe. Majaliwa yanaelekeza Hekari 1200 kati 1598 zitarejeshwa kwa wananchi kwa ajili ya shughuli hizo za maendeleo na Hekari 398 zitabaki kwa Mwekezaji Laizer Mihanga ambaye alikuwa anamiliki shamba hilo hapo awali.  

‘’…Sasa Serikali imechukua hatua zifuatazo, kwanza lile shamba limefutwa ni mali ya  Serikali, kwa hiyo hakuna mwenye kusema ana shamba lake…’’ amesema Shigela.

Aidha, Shigela amefuta kesi zilizokuwepo baina ya Mihanga na wananchi zinazohusu shamba la Chanzuru, amepiga marufuku mwananchi yoyote kukamatwa ama kuondolewa wakati anafanya shuguli zake za kimaendeleo alizokuwa anazifanya ndani ya shamba hilo na kuwataka wananchi hao  kuwa huru kuendelea na majukumu yao bila kubugudhiwa.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya shamba hilo kuchukuliwa na Serikali na kulitoa kwa wananchi kazi inayofuata ni kuweka utaratibu wa namna ya kuligawa kwa wananchi hao ili kuweka usawa katika kugawana badala kila mmoja kujitwalia eneo kwa ukubwa anaoutaka hali itakayoleta tena migogoro kwao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga amekiri kupokea maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa ya kufuatilia utekelezaji wa maagizo hayo ya Waziri Mkuu na kumuhakikishia kudumisha ulinzi, Amani na usalama kwa wananchi wa Chanzuru na pamoja na mali zao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa Kijiji cha Chanzuru wameonesha furaha yao juu ya uamuzi wa Serikali wa kufuta shamba hilo akiwemo Ally Omary, huku wakimuomba Mkuu wa Mkoa kuunda kamati kwa ajili ya kuweka mipaka ya eneo lote la Ekari 1,200 walilopewa ili kuepusha  migogoro inayoweza kujitokeza tena.

Naye, Mkude Omary, licha ya furaha na pongezi kwa Mkuu wa Mkoa, amemuomba Hekari 368 zilizobaki kwa ajili ya Mwekezaji Laizer zirudishwe kwa wananchi kwa sababu Mwekezaji huyo alikuta Mikonge katika shamba hilo ambayo ilikuwa linalimwa na wananchi wa kijiji hicho.

Mwekezaji Laizer Mihanga ambaye muda mwingi amekuwa akidai kuwa shamba la Mikonge la chanzuru lenye ukubwa wa Ekari 1,598 ni mali yake kwa sasa amepewa jumla ya Ekari 398 kwa ajili ya kuendelea na shughuli za kilimo cha zao hilo la Mkonge alichokuwa akikiendesha.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.