• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANANCHI WA KIBWAYA MOROGORO WAMKUNA RC SHIGELA , ACHANGIA MIFUKO 50 YA SARUJI

Posted on: June 22nd, 2022

RC Morogoro achangia mifuko 50 ya Saruji kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kibwaya

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameunga mkono juhudi za wananchi wa Kijiji cha Kibwaya kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mkoani humo kwa kuchangia mifuko 50 ya saruji baada ya wananchi hao kujenga boma la zahanati kwa nguvu zao.



RC Martine Shigela

Martine Shigela amefikia hatua hiyo Juni 22 mwaka huu alipoutembelea mradi huo na kuridhika na ubora wa jingo hilo pamoja juhudi za wananchi za kujenga zahanati hiyo ambayo iko katika hatua ya umaliziaji huku wakianza ujenzi wa nyumba ya mganga jambo lililomsukuma Kiongozi huyo kuchangia mifuko 50 ya saruji.

“Sasa madamu mmejitolea na mimi nitawachangia mifuko ya simenti hamsini ili ujenzi huo uanze mara moja, kwa hiyo shukrani hizo tutamfikishia Mhe.Rais na ninyi mnajua siku zote mwenye nacho ndiye anayeongezewa” amesema Martine Shigela.



jengo la zahanati lya Kibwaya ililojengwa kwa nguvu za wananchi wa kijiji hicho likiwa kwenye hatua za umaliziaji

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Kibwaya akiwemo Bw. Juma Kisiga wamemshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea fedha shilingi milioni 50 za kumalizia jengo la zahanati ambalo walianza kujenga mwaka 2010 na kukamilika mwaka 2013 bila mwendelezo wowote hadi sasa Mhe. Samia alipopeleka fedha za kumalizia jengo hilo.

“Hili jengo lilianza kujengwa mwaka 2010 likaisha  2013, tangu hapo likakaa kimya mpaka sasa awamu hii ya Mama Samia ndio kazi hii inaendelea kufanyika tena kwa ubora, juu ya hilo tunaomba salamu za asante zifike ngazi zote za Serikali zilizoshiriki kutufanikishia jambo hili” amesema Bw. Juma Kisiga.


Mhe. Shigela akikagua ujenzi wa Jengo la Zahanati ya Kibwaya

Katika hatua nyingine, wananchi wa Kijiji hicho wamelalamikia mradi wa maji uliojengwa kijijini hapo na kugharimu Shilingi 610,000,000/=  ulioanza kujengwa tangu mwaka 2015 lakini mradi huo bado hauna tija kwa wakazi wa eneo hilo kwa kuwa maji yanatoka kwa kusua sua.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Rehema Bwasi

Sehemu ya Wahe, Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro wakiwa kwenye kikao Maalum cha kujadili hoja za Mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali  - CAG Juni, 22 2022

Kwa sababu hiyo, Mkuu wa Mkoa Martine Shigela amewatahadharisha wote wanaotuhumiwa kuhusika na ujenzi wa mradi huo wa maji na kwamba kama maelezo yaliyotolewa na wananchi yako sahihi, basi wajiandae kuzitapika fedha zote za mradi huo walizozitafuna.

kutoka Kushoto, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Martine Shigela na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo, wakiwa kwenye kikao muda mfupi kabla ya kutembelea jengo la zahanati ya Kibwaya

Ameongeza kuwa, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan ina dhamira ya dhati ya kumtua mama ndoo kichwani na kwa kuwa makosa ya jinai hayaozi wahusika wa mradi huo watatafutwa ili wakamilishe mradi huo ili ulete tija kwa wananchi.

Hata hivyo, amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo kufuatilia kwa karibu changamoto za mradi huo kupitia kwa kwa Wakala wa Maji Mijini na Vijijini RUWASA ili kujua tatizo haswaa la mradi huo kutotoa maji.

Kushoto, ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja

Baadhi ya watendaji wa Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro, katikati ni Dr. Rozaria Rwegasira Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na uzalrishaji Mali kulia ni Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mita Bw. Leopord Ngirwa


Baadhi ya Viongozi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro (DAS), Afisa Usalama wa Taifa Wilaya (DSO) na Kamanda wa Polisi wa Wilaya hiyo (OCD)

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.