• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi wa Mabula waaswa kulinda Mradi wa maji.

Posted on: November 26th, 2020

Wananchi wa Kijiji cha Mabula Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wameaswa kutunza na kulinda mradi wa maji uliofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la World Vision ili kuuwezesha mradi huo kudumu kwa muda mrefu na kuwaletea maendeleo yao.

Ushauri huo kwa wananchi wa Kijiji hicho umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare Novemba 25 mwaka huu wakati wa uzinduzi wa Mradi huo baada ya kukamilika na kuwapunguzia wanawake mzigo wa kutafuta maji umbali mrefu.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema ili mradi huo uwe endelevu ni lazima Kamati ya watumia maji iundwe na hiyo ndiyo itaratibu namna nzuri ya kuuendeleza mradi na itaratibu pia namna ya kuutunza ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kisima cha maji kwa ajili ya mradi huo kinazungushiwa uzio.

“haya maji tusipoyapangilia vizuri kuna siku yatakatika, na kamati ile iratibu namna ya kupata koki mara itakapokuwa imeharibika… Sasa namna ya kufanya ni kuandaa kamati ya maji ya kijiji chini ya viongozi tuliowachagua” alisema Sanare. 

Pamoja na ushauri alioutoa juu ya kuunda Kamati kwa ajili ya kusimamia mradi na kuufanya kuwa endelevu kwa kuwapa elimu wananchi kuchanga fedha kidogo itakayoendeleza mradi, Loata Sanare amewaonya viongozi wa Kijiji kutoingilia majukumu ya kamati itakayoundwa  na kufuja fedha za mradi huo zitakazochangwa na wananchi kwani wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi kutoka Word Vision Bw. Donasian Severine amesema lengo la Mradi wa maji katika Kijiji cha Mabula ni kushirikiana na jamii na wadau wengine kuhakikisha maisha ya mtoto yanastawi katika Nyanja zote za elimu, Afya na Ulinzi na Usalama. Huku akibainisha kuwa mradi huo utanufaisha wakazi 3,322 wa vijjij wa kijiji cha mabula.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameishukuru shirika lisilo la kiserikali la Word Vision kwa uhisani wanaoutoa katika Wilaya ya Kilosa katika kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo yao kwenye sekta za Elimu, Afya na sekta nyingine ndani ya Wilaya hiyo hususan katika Tarafa za Magole na Ulaya. 

Naye mwakilishi wa RUWASA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joshi Chumu amesema mradi huo umetekelezwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi 220 Mil. huku akiahidi kutoa Elimu kwa wananchi namna ya kuunda jumuiya kwa lengo la kuendeleza Mradi huo.

Mradi huo unaofadhiliwa na World Vision unatekelezwa katika Kata sita na vijiji 21 ndani ya Wilaya ya Kilosa Mkoani humo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.