• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi wa Malinyi wamlilia RC Shigela.

Posted on: June 14th, 2021


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Mkoani Morogoro wamemuomba Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela kutatua kero mbalimbali wanazokumbana nazo ili kurahisisha shughuli za maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Wananchi wametoa maombi hayo June 12, mwaka huu katika Mkutano wa hadhara na wananchi uliofanyika Wilayani humo  kwa lengo la kusikiliza kero wanazokumbana nazo na kuzitolea maamuzi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao akiwemo Ndg. Hassan Issa, amesema wanakabiliwa na miundombinu mibovu ya  barabara ya Malinyi – Ifakara hali inayopelekea kushindwa kusafirisha bidhaa zao kutokana naubovu wa miundombinu hiyo hususan kipindi cha masika.

Aidha, Ndg. Issa ameiomba Serikali iwatengenezee barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili waweze kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi, hivyo kukuza uchumi wao, Mkoa na taifa kwa jumla.

‘’…..Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, kwa muda mrefu sasa tuna changamoto ya barabara, wakandarasi ambao walipewa barabara hii huonekana pale tu mvua zinapoanza kunyesha, nyakati za kiangazi hawashughuliki na barabara hii, kiukweli tunateseka sana,.’’ amesema Ndg. Issa.

Sambamba na hayo, ametoa ombi kwa Mkuu huyo wa Mkoa kuwakamilishia vituo vya Afya ili kuwasogezea huduma karibu wananchi ambao wanatembea umbali mrefu kufuata huduma za matibabu.

Naye Anitha Bondwa, amebainisha kero ya wauguzi ambao wanawachangisha fedha kwa ajili ya matibabu licha ya kuwa na bima za Afya ambazo kwa mujibu wa maelezo yake haziwasaidii pindi wanapohitaji huduma za matibabu katika vituo vya Afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mathayo Masele amesema hadi sasa wamefanikiwa kupata zaidi ya shilingi Milioni 150 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Malinyi, Bilo na zahanati ya Madabadaba  ambazo zikikamilia zitasaidia kuondoa changamoto ya umbali mrefu wa kufuata huduma za Afya.

Akizungumza na wananchi wa Malinyi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela, ametoa maelekezo mbalimbali na kutatua changamoto za wananchi hao ambapo amemtaka Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kufuta utaratibu wa wagonjwa kulipa pesa kwa ajili ya matibabu na kuagiza Halmashauri kusimamia suala hiyo.

‘’Kuanzia leo sitaki kusikia wala kuona wananchi wanalipa hiyo pesa ili watibiwe, haiwezekani mnawahamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya Afya halafu muwatoze fedha, hiyo pesa ambayo walikuwa wanaitoa kwaajili ya mlinzi, Halmashauri iwajibike’’ Amesema Shigela.

Katika hatua nyingine, Shigela ametoa ufafanuzi juu ya ujenzi wa barabara ya Malinyi - Ifakara ambapo amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania iko mbioni kutengeneza barabara hizo ili kuwarahisishia maendeleo wananchi wa Wilaya hiyo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.