• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

wananchi wa matuli waondokana na changamoto ya mawasiliano

Posted on: November 30th, 2021

Wananchi wa Matuli Wilayani Morogoro waondokana na changamoto ya mawasiliano

Wananchi wa Kata ya Matuli Wilayani Morogoro Mkoani humo wameondokana na changamoto ya kukosa mawasiliano ya simu baada ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa fedha shilingi Milioni 125 kwa ajili ya kujenga mnara wa simu wa Kampuni ya Aiterl.

Hayo yamebainika Novemba 30 mwaka huu wakati wa uzinduzi wa Mnara huo uliojengwa katika Kijiji cha Matuli Kata ya Matuli Wilayani Morogoro, na kuzinduliwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Ashatu Kijaji (MB)huku wananchi wakisimulia namna walivyokuwa wakipata changamoto katika kupata mawasiliano hayo ya simu.

Wamesema, awali wananchi hao walikuwa wanatumia makopo yaliyotundikwa kwenye mti ili kupata mtandao na kila aliyehitaji kupata mawasiliano ya simu alilazimika kutumbukiza simu yake kwenye moja ya kopo lililotundikwa juu ya mti na kuongea simu yake ikiwa imemening’inizwa kwenye mti huo.

Siku ya leo wananchi hao wameonesha furaha yao mara baada ya kuzinduliwa kwa mnara huo wa simu na kuanza kupata mtandao huku wakiongea na ndugu, jamaa na marafiki zao pasipo kutumia makopo bali wakiongea huku wakitembea barabarani, hivyo wameipongeza Serikali ya awamu ya sita na Mbunge wao Mhe. Hamis Taletale Maarufu kama Babu Tale kwa kupambana na kuwaondolea kero hiyo.

“Mbunge wetu katufanyia mambo hayo mazuri tunashukuru sana, tunampa pongezi na Serikali yetu kwa ujumla tunashukuru sana” alisema mwananchi mmoja wa Matuli aliyejulikana kwa jina la Omary Kamete.

Akiongea na wananchi wa Kijiji cha Matuli na vijiji jirani, wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa Mnara, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Ashatu Kijaji ameeleza kazi ya Wizara yake kuwa ni kuhakikisha wanawafikishia wananchi huduma ya mawasiliano kwa asilimia kubwa na kwa uhakika ndani ya miaka mitano ya Serikali iliyoko madarakani.

“Na tunakwenda kuhakikisha ibara hizi mbili nilizozitaja tunazitekeleza kwa nguvu zetu zote….ibara hizi mbili zinatutaka tufanye yafuatayo; moja watanzania tuwafikishie huduma za mawasiliano kwa asilimia mia moja ndani ya miaka mitano hii…” amesema Dkt. Ashatu Kijaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema, pamoja na kutambua Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kupeleka fedha nyingi za maendeleo Mkoani humo ikiwa ni pamoja na fedha za Barabara, Vituo vya Afya, Umeme na Fedha za Ujenzi wa Vyumba vya madarasa bado amesema kuwa ujenzi wa mnara huo, utaleta chachu kwa Familia na jamii nzima kwa ujumla hasa kiuchumi.

Naye Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote hapa nchini (UCSAF) amesema jukumu la kupeleka mawasiliano kwa wananchi ni jukumu lao na hadi sasa wamekwisha peleka huduma hiyo katika kata laki moja na elfu sitini na nane kwa nchi nzima huku akiahidi kuwa UCSAF imejizatiti kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi ikiwa ni pamoja na kuongeza matumizi ya Internet kutoka 45% hadi kufikia 80%.

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya simu za Mkononi – Aitel, Jackson Mmbando amesema pamoja na changamoto ya ugumu kupata mawasiliano waliokuwa nao wananchi wa Matuli, wananchi hao walikuwa kwenye hatari kubwa hususan kwa upande wa usalama wa fedha zao.

Amesema wakala aliyekuwa anafanya kazi ya kutoa ama kuweka fedha ndani ya kijiji hicho alikuwa mmoja, na watu wote walijua kuwa wenye shida ya kutoa au kuweka fedha ni lazima wamtumie wakala huyo pekee jambo ambalo halikuwa jema kwa usalama wa fedha zao, hata hivyo amesema kampunia ya Airtel imemaliza changamoto hiyo na wako salama na huru sasa kutumia mtandao huo wa Airtel.

Imeelezwa kuwa jumla ya shilingi za kitanzania milioni 350 zimetumika katika ujenzi wa mnara huo hadi kukamilika kwake.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.