• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi wa Namawala wamlilia RC Shigela

Posted on: June 25th, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Namawala  Wilayani Kilombelo Mkoani Morogoro wamemuomba Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela kutatua mgogoro wa  shamba baina yao na mwekezaji mzawa anayejulikana kwa jina la Said Kambenga ambapo  kila upande unadai kuwa shamba hilo ni mali yake.

Wananchi hao wametoa ombi hilo hivi karibuni walipokutana na Mkuu wa Mkoa huyo na kumueleza mgogoro huo ambao umedumu kwa zaidi ya miaka mitano bila kupatiwa ufumbuzi huku wananchi hao wakilalamikia kupigwa, kushtakiwa mahakamani, kutishiwa maisha na mwekezaji kila wanapojihusisha na kilimo ndani ya shamba hilo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao akiwemo Bi. Shamila Ramadhani amesema kila msimu wa kilimo wanapoenda kulima katika eneo hilo ambalo walipewa na kijiji, Kambenga amekuwa akiagiza polisi kuwazuia wasiingie shambani au kuwapeleka rumande ama kuwafikisha mahamani na kuwafungulia kesi ya jinai kwa kosa la kulima katika shamba lake.

‘’…Hana vithibitisho vya kuonesha uhalali wa kumiliki hekari 1000 kama mwekezaji,  akiambiwa aoneshe hati  ya umiliki wa hekari 1000 hana,  ana hati ya umiliki wa hekari 100 sasa tunashangaa inakuwaje anadai hekari 1000’’… alihoji Bi. Shamila.

Wakielezea chanzo chake, wananchi hao akiwemo Melisa Gozibert, amesema mgogoro huo umeanza mwaka 1996 ambapo mwaka 2020 waliwasilisha kero hiyo kwa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara Mkoani Morogoro ambapo alimuagiza Mkuu wa Mkoa kuitisha kikao cha kutatua mgogoro huo.

Pamoja na Mkuu wa Mkoa kutekeleza agizo la kukutanisha pande hizo mbili ili kupata suluhu, bado hakukuwa na mwafaka kwa kuwa uchunguzi wa kupata nyaraka za umiliki wa shamba hilo ulihitajika zaidi ili kujiridhisha zaidi kuhusu mmiliki halali.

Kwa sababu hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare kwa wakati huo alitoa maelekezo kwa Kambenga kutowasumbua Wananchi wenye mazao yao ndani ya shamba hilo hadi watakapovuna huku akimtaka naye kusitisha kuendelea kulima.

Aidha, Melisa amebainisha kuwa kijiji cha Namawala hakina mamlaka ya kumpa mwekezaji hekari 1000 na hakuwahi kulipia kodi ya shamba hilo tangu mwaka 2009 hadi sasa.

Kwa upande wake anayedaiwa ndiye mmiliki shamba hilo lenhye hekari 1000 Said Kambenga, amesema ana hati zote za kumiliki shamba hilo ambalo mahakama ya Ardhi ya Mkoa huo ilimpa umiliki wake tangu mwaka 2010 akiwepo Mwenyekiti wa Kijiji hicho ambaye kwa sasa ni marehemu.

Katika hatua nyingine, Kambenga amesema kutokana na wananchi kumuingilia katika shamba hilo na kuharibu mazao yake aliamua kuajiri kampuni ya ulinzi imsaidie kulinda shamba na kutoharibu mazao yake.

Akihitimisha mvutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewataka pande zinazohusika kuwa watulivu ili aunde timu itakayohusisha Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Wataalamu wa Ardhi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na Uongozi wa kijiji, kwa lengo la kubaini maeneo yaliyolimwa ndani ya shamba hilo pamoja na wamiliki wake.

‘’…Tutabainisha maeneo yenye mgogoro ili tuje tuyatafutie ufumbuzi, kwenye maeneo ambayo hayana migogoro, yale yenye migogoro tuyatafutie ufumbuzi na yale ambayo hayana tuyaache kwenye mlolongo mwingine…’’ amesema Shigela.

Sambamba na maagizo hayo, Shigela ameagiza kusiwepo na mtu yeyote wa kufanya shughuli zozote za kilimo katika shamba hilo mpaka pale kamati yake itakapofanya utafiti na kujiridhisha na kuwaletea majibu ya kamati yake na kuhitimisha mgogoro huo rasmi.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.