• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi waunga Mkono jitihada za JPM, waunganisha nguvu kujenga Shule ya Sekondari.

Posted on: January 4th, 2021

Wananchi wa Kata ya Boma katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wameunga Mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuunganisha nguvu zao na Halmashauri kujenga Shule mpya ya Sekondari inayotarajiwa kukamilika kabla ya tarehe 28 Februari mwaka huu kwa kujenga vyumba 10 vya madarasa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  hivi karibuni wananchi wa Kata ya Boma, wamesema wamesumbuka kwa muda mrefu kutafuta sehemu ya karibu  kwa ajili ya ujenzi wa Shule hiyo, hivyo wameishukuru serikali kwa kuwapatia eneo ambalo lipo katika kata  yao na kuahidi kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa shule hiyo.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Boma Athuman Omary, amesema ameunga mkono jitihada za Serikali kutokana na imani kubwa aliyo nayo juu ya Serikali ya awamu ya tano, laikini pia kwa lengo la kuwezesha miundombinu rafiki kwa wanafunzi ili wasitembee umbali mrefu kufika Shuleni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro,  Afisa Elimu wa Halmashauri hiyo Dkt. Janeth Balongo amesema Shilingi Mil.578 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo huku shilingi Mil. 100 zikiwa tayari zimewekwa katika akauti yao kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo.

Aidha, Dkt. Balongo amesema shule hiyo itakuwa ni shule shikizi kwa sasa na kwamba itachaguliwa shule moja ambayo itailea kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa mwaka huu na baada ya kukamilisha ujenzi itakuwa shule maalumu kwa ajili ya masomo ya  Sayansi.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo aliyefika eneo la ujenzi kwa lengo la kukagua na kuhamasisha ujenzi huo, ameipongeza Halmashauri hiyo kwa uamuzi wa kujenga shule mpya na kwa ubunifu wao wa kuamua kujenga madarasa hayo kwa mtindo wa ghorofa.

“... Na leo nimesikia Manispaa wanaanzisha ujenzi wa shule mpya ambayo kabla ya Februari 28 mwaka huu itakuwa na vyumba kumi vya kutosha, nawapongeza sana Manispaa…..lakini bado wanasema kwa sababu sisi tupo Mjini hatuwezi kujenga ujenzi wa kawaida, watajenga majengo ya ghorofa tatu tatu hapa… alisema Mhandisi Kalobelo.

Aidha, Mhandisi Kalobelo amesema shule hiyo itakuwa ni ya mfano ambayo itahusika na masomo ya Sayansi lakini pia wanafunzi watapata nafasi ya kusoma Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wakiwa shuleni hapo.

Morogoro ni miongoni mwa Mikoa ambayo imefanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa darasa la saba ambapo mwaka huu 2020 imeshika nafasi ya nane Kitaifa kutoka nafasi ya 16 mwaka 2019. Mkoa unaendelea kujipanga kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu darasa la saba 2020 wanajiunga na kidato cha kwanza mapema mwaka huu.

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.