• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi waunga Mkono serikali kuwaondoa waliovamia Hifadhi.

Posted on: December 17th, 2020

Waananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Mkoani Morogoro wameafiki agizo la Serikali la kuhama katika eneo la hifadhi  katika Bonde la Mto kilombero  Ili kumuunga mkono Dkt. John Pombe Magufuli katika azma yake ya ujenzi wa mradi wa umeme wa Mwalimu nyerere ambao asilimia 62 ya Maji yatakayoendesha mradi huo yanatokana  na  hifadhi hiyo.

Hayo yamebainishwa Disemba 16 Mwaka huu na baadhi ya Wananchi wa Wilaya hiyo, walipohojiwa na vyombo vya habari baada ya Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mathayo Maselle kueleza azma ya Serikali ya Wilaya hiyo kukusudia kuwaondoa wavamizi wote wa bonde hilo la hifadhi alipokuwa akifungua kikao cha kwanza cha wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi.

Wananchi hao akiwemo Bi. Maija Amrani wa Kijiji cha Ngohelanga wamesema hawaungi mkono wananchi wenzao kuendelea kufanya shughuli za kibinamu ndani ya eneo la hifadhi kwa kuwa wanaharibu vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na mradi mkubwa wa kufua umeme wa Mwalimu Nyerere ulioazishwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unaenda kuleta unafuu kwa wananchi katika kupata nishati ya hiyo ya umeme.

“….lakini ilishasemwa kwamba wanaokaa karibu na vyanzo watoke, na hasa wale  wanaokaa kuanzia chini ya mwaka 2017 kurudi chini wale wote wa nyuma watoke, lakini lile la mwaka 2012 kuja huku lina ruhusa watu waendelee kulitumia, kwa hiyo ni vyema kutoka katika hifadhi ili kuunga mkono jitihada za Rais wetu….” Amesema Amrani

Naye January Silvester amesema eneo hilo limekuwa likivamiwa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali huku baadhi yao wakijimilikisha maeneo makubwa katika hifadhi hiyo kinyume na sheria, hivyo wanaunga mkono agizo la serikali la wavamizi hao kuondoka katika hifadhi ya Bonde la Mto Kilombero licha ya changamoto watakazokumbana nazo katika kuhamia maeneo mapya.

Akizungumza katika Kikao cha baraza hilo Mkuu wa Wilaya hiyo Mathayo Masele aliyekuwa Mgeni rasmi amesema eneo la hilo  la hifadhi linachangia kwa asilimia 62 ya maji yote yanayoelekea katika bwawa la Mwalimu Nyerere, hivyo wananchi wanaoishi katika hifadhi hiyo hawana budi kuhama ili kupisha ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa  Wilaya alitaja mikakati iliyopo ya kuhakikisha watu waliovamia maeneo  ya hifadhi wanaondoka kwa amani ni pamoja na kutoa Elimu juu ya umuhimu  wa Bonde hilo la Mto Kilombero.

Mikakati mingine ametaja kuwa ni kutoa Elimu juu ya kubadili mtindo wa kilimo, kulima eneo dogo lakini linaloweza kutoa mavuno ya kutosha, kubadili aina ya mazao ya kulima badala ya  kuamini kilimo cha mpunga pekee. Mkakati mwingine ni wananchi  kujikita katika kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia Skimu za umwagiliajo zilizopo na kuanzisha nyingine mpya.

Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro Crister Njovu (kulia) na Marcelin Ndimbwa wakijadili jambo wakati wa Kikao hicho

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Pius Gerlad amesema Serikali iangalie uwezekano wa kutoa eneo la kipande cha hifadhi linalopatikana kati ya mipaka ya mwaka 2012 na 2017 ili liwasaidie wananchi watakao hamishwa kutoka maeneo ya hifadhi hiyo.

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.