• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANAWAKE MOROGORO WANA MCHANGO KATIKA MAENDELEO.

Posted on: March 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema miongoni mwa makundi yanayochangia ukuaji wa Uchumi wa Mkoa huo ni kundi la wanawake, hii ni kutokana na kundi hilo kuwa na ushiriki mkubwa katika shughuli za kimaendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Mhe. Malima amesema hayo Machi 8, 2024 kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya shule ya Msingi K/ Ndege iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amewapongeza Wanawake wa Mkoa huo kwa jitihada za kuendeleza maendeleo ya Mkoa huo na kubainisha kuwa Mkoa unasongambele kwa kasi pia amesema Mkoa una malengo mbalimbali ya kimaendeleo ambapo wananwake hao ndiyo msingi wa kuyafikia malengo hayo.

“...niwapongeze akina mama wote wa Morogoro kwa kazi na jitihada mnazofanya katika kuleta maendeleo ya Mkoa wetu...akina mama ni msingi wa mafanikio ya Mkoa wetu wa Morogoro...” amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mhe. Malima amesema Taifa lisiloheshimu mchango na nafasi ya wanawake katika shughuli za maendeleo basi Taifa hilo litakuwa limedumaa huku akieleza kuwa uwekezaji kwa wanawake unaibadilisha jamii moja kwa moja.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa ametumia maadhimisho hayo kuwataka wananchi wa Mkoa huo kuachana na vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ubakaji na ulawiti huku akiweka bayana kuwa Mkoa umejipanga kwa dhati kukomesha vitendo hivyo.

Sambamba na hilo amezitaka taasisi zinazohusika na utoaji wa haki kuendelea kutoa elimu juu ya haki za wanawake hususan walio katika mifumo ya ukatili wa kijinsia.

Naye Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro Bi. Susan Kihawa amesema Mahakama ya Tanzania imefanya maboresho mbalimbali kwenye sheria na haki za wanawake huku akisema kuwa ukombozi wa kifikra na Elimu madhubuti ni jambo linalotakiwa kutiliwa mkazo ili wanawake waweze kutambua haki zao.

Akisoma risala kwa niaba ya wanawake wa Mkoa huo Bi. Sophia Kalinga amesema uwekezaji kwa wanawake ni sawa na kuwekeza kwa jamii kwani mwanamke ni mlezi wa familia anayesimamia malezi na maadili kwa Watoto lakini pia anatunza uchumi wa familia, hivyo jamii inapaswa kuwa na mtazamo chanya kwa wanawake kuwa wanauwezo sawa na wanaume.

Aidha, Bi. Sophia ameishukuru Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga shule maalumu za wasichana kila Mkoa ambapo Morogoro ni miongoni mwa mikoa iliyonufaika hivyo wanawake watapata fursa ya elimu ambayo ndiyo mkombozi wa mwanamke.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.