• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wanufaika TASAF watakiwa kujitegemea

Posted on: December 14th, 2021

Wanufaika wa TASAF kuwa na mwelekeo wa kujitegemea.

 

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mpango wa kunusuru Kaya Masikini Tanzania - TASAF Dkt. Charles Mwamwaja amesema kuwa mwelekeo wa TASAF kwa sasa ni kuona kuwa wanufaika wa mpango huo wanakua, wanaendelea na mwisho wanajitegemea kiuchumi.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mpango wa kunusuru Kaya Masikini Tanzania - TASAF Dkt. Charles Mwamwaja na ujumbe wake akiongea na wananchi wa kijiji cha Mkambarani

Dkt. Mwamwaja amesema hayo Disemba 13 mwaka huu wakati wa ziara ya Wajumbe wa Bodi hiyo Moani humo ambapo Pamoja na shughuli nyingine wametembelea miradi inayotekelezwa na TASAF ukiwemo mradi wa zahanati iliyojengwa na TASAF awamu ya kwanza katika Kijiji cha Mkambarani.

baadhi ya wajumbe wa Bodi wakiwa katika kikao hicho


Akiongea na wananchi wa Kijiji cha Mkambarani kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Dkt. Mwamwaja ameonesha kufurahishwa na uanzishwaji wa vikundi vya ujasiliamali ndani ya wanufaika wa Mpango huo na kwamba kupitia vikundi hivyo wanaweza kunufaika na mikopo inayotolewa na Halmashauri au hata ya kutoka Serikali Kuu hivyo kujinusuru na umaskini waliokuwa nao awali.

baadhi ya wanufaika wa kijiji cha Mkambarani

Kwa sababu hiyo Dkt. Mwamwaja amewahamasisha wanufaika hao kuendeleza vikundi hivyo ambavyo vingine vinatengeneza  sabuni na kuwahakikishia kuwa huo ndio mwelekeo wa TASAF kutaka wanufaika kutumia kile kidogo wanachopata kukiendeleza  na mwisho waweze kujitoa kwenye umasikini na kujitegemea.

“huo ndio mwelekeo, tungependa hawa wenzetu tuwaunge mkono, huko wanakoelekea wataanzisha vikundi…. vikikua vitafika mahala vitafanya ujasiliamali mdogomdogo…..vitanufaika na mikopo inayotolewa na Halmashauri na baadae inayotolewa na Serikali” amesema Dkt. Mwamwaja

 Mwenyekiti akinunua sabuni zilizozarishwa na moja ya vikundi vilivyoanzishwa kujinusuru na umaskini

Pia amesisitiza kuwa furaha ya mzazi sio tu kumlea mtoto zaidi kuona mtoto anafika mahali anajitegemea, na hilo ndilo lengo la TASAF la kuwataka kuwanusuru wanufaika kwa kuwapa fedha kidogo na maarifa hatimaye waweze kujitegemea wenyewe.

“neno letu ni kwamba tutahakikisha tunamlea, anakua ili kesho na kesho kutwa furaha ya mzazi si kumwona mtoto anajitegemea! kwa hiyo tutamlea tutahakikisha anakua ili kesho na kesho kutwa na yeye aanze kujitegemea” amesisitiza Dkt. Mwamwaja

 sabuni zinazotengenezwa na kikundi baada ya kupata mafunzo na utaalamu chini ya uratibu wa TASAF

Aidha, amewatoa hofu wanufaika hao kuwa, TASAF itaendelea kusaidia walengwa wanaokizi vigezo kwa lengo la kupiga vita umasikini na hatimaye kuona wanajikwamua na kisha kujitegemea kiuchumi.

Akiwa katika kikao cha Pamoja na uongozi wa Mkoa na Wilaya katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Mwamwaja amesema miradi inayoanzishwa na TASAF ni miradi ya Serikali hivyo inatakiwa kushughulikiwa kama miradi mingine ya Serikali kwa kuwa lengo la TASAF ni kuondoa adui umaskini miongoni mwa watanzania lengo ambalo linatekelezwa pia na Serikali Kuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela Pamoja na kutoa shukrani kwa Wajumbe wa Bodi ya TASAF kutembelea Mkoa huo, amewataka Waratibu wa TASAF Wilaya na Mkoa Mkoani humo kuendelea kutoa Elimu muda wote juu ya vigezo vinavyomuingiza mnufaika kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando

Amesema kuacha wananchi peke yao kuchaguana kutaendeleza malalamiko kwa sababu wengeni wanaweza kuingizwa kwenye mpango kisiasa au kwa ushawishi hivyo kutotatua malalamiko ya suala la TASAF kama ambavyo hujitokeza karibu kila mikutano ya hadhara.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini ngazi ya Mkoa, Mratibu wa TASAF Mkoa wa Morogoro Jacob Kayange ametaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana kwa wanufaika wa mpango huo kupitia ruzuku wanayopata kuwa imewasaidia baadhi yao kupata maeneo ya kulima hivyo kuongeza kipato.

Mratibu TASAF Mkoa wa Morogoro Bw. Jacob Kayange akitoa maelezo juu ya utekelezaji wa TASAF Mkoani humo

Mafanikio mengine ni Pamoja na wanufaika kuanzisha biashara ndogo ndogo, kujiunga na CHF kwa lengo la kujiwekea akiba kwa ajili ya matibabu, kuhudumia mahitaji ya Watoto shuleni na mpango umewezesha kuongeza mahudhurio mazuri ya Watoto shuleni kutokana na kaya hizo kupata ruzuku ya fedha kutoka kwenye mpango huo.

Zahanati ya Mkambarani iliyojengwa na TASAF awamu ya kwanza

Ujenzi wa maabara na Wodi ya mama na mtoto katika zahanati ya Mkambarani ukiendelea

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya TASAF Taifa Dkt. Charles Mwamwaja akikagua ujenzi wa Miundombinu inayoendelea kujengwa katika zahanati ya Mkambarani

Wakitoa ushuhuda wao mbele ya Wajumbe wa Bodi ya TASAF, wanufaika wa mpango huo kutoka Kijiji cha Mkambarani wametoa shukrani zao kwa Bodi hiyo kwa kuwajengea zahanati ya Mkambarani ambayo kwa sasa  imeingiziwa fedha tena zaidi ya shilingi Mil. 188 kwa ajili ya kujenga maabara na wodi ya mama na mtoto katika zahanati hiyo.

shuhuda wa Mpango wa kunusuru kaya masikini akishuhudia jinsi alivyofaidika na mpango huo

Aidha, wamekiri kuwa TASAF imewasaidia kwa kiwango kikubwa, kwanza kwa kuwapa fedha zilizowawezesha kuanzisha miradi kwa mtu mmoja mmoja na baadae kuazisha vikundi vya Pamoja vya ujasiliamali vya Faraja na Tushikamane ambavyo vinawasaidia katika kusomesha Watoto na kujipatia mahitaji muhimu.

Shuhuda

Ombi lao wananchi hao ni moja tu, TASAF iendelee kuwalea lakini pia kuwaingiza kwenye mpango huo wazee wengine waliopo katika Kijiji cha Mkambarani na maeneo mengine hasa wale wanaokidhi vigezo vya kuingia kwenye mpango ili kuondoa malalamiko ambayo yameendelea kuwepo ndani ya TASAF.

Mpango wa TASAF awamu ya kwanza katika Mkoa wa Morogoro umetekelezwa katika Halmashauri mbili za Morogoro na Ulanga, TASAF awamu ya pili ilihusisha halmashauri sita  za Morogoro DC, Manispaa ya Morogoro, Kilosa, Kilombero, Ulanga na Mvomero na awamu ya tatu mpango ulianza rasmi mwaka 2012 na Morogoro umeanza mwaka 2013  na kwa awamu hiyo jumla ya shilingi Bi.10.23 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo kwa walengwa wapatao 47,124.

Baadhi ya viongozi wakimsikiliza Dkt. Mwamwaja akiongea na wanufaika wa Mkambarani. kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Mkoa wa Morogoro Anza Amen Ndossa

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.