• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wanufaika wa mikopo ya 10% watakiwa kurejesha kwa wakati.

Posted on: April 17th, 2025

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi amewataka wanufaika wa mikopo ya 10% kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwapa nafasi wanufaika wengine kukopa kwa ajili ya kukuza biashara zao kwa maslahi yao na Taifa.


Kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa uhuru amesema hayo Aprili 17, mwaka huu wakati wa kuona kituo cha Enlight development organisation (EDO) kinachowawezesha vijana kiuchumi na kupinga ukatili kwa watoto kilichopo Halmashauri ya Mji Ifakara Wilayani Kilombero.


Akifafanua zaidi, Ndugu Ismail amesema mikopo hiyo isiyokuwa na riba imetengwa kwa ajili ya vijana, watu wenye ulemavu pamoja na wanawake ili kukuza vipato vyao hivyo, amewataka wanaochukua mikopo hiyo kurejesha kwa wakati ili wahitaji wengine waweze kukopa.


"... vijana wanaokopeshwa fedha wanatakiwa wazirejeshe ili wengine waweze kutumia fedha hizo..." amesema Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.


Katika hatua nyingine, amelipongeza dawati la jinsia kwa kufanya kazi kwa haki na kwa ufanisi mkubwa hivyo amewataka wataalam hao kuhakikisha wananchi wanaoshinikizwa na vitendo vya unyanyasaji wanasimamiwa na kupata haki yao ili kuondoa vitendo hivyo kuendelea ndani ya jamii.  


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kituo cha EDO Bi. Josephine Saidi amesema kituo hicho kimekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia wanawake wa hali ya chini wanaokumbana na changamoto ya maisha pamoja na ukatili wa kijinsia hivyo kituo hicho kinawapa mafunzo ya kilimo cha mbogamboga na matunda ili kupata uwezo wa kwenda kujitegemea kiuchumi.


Naye, mnufaika wa mradi huo Bi. Makrina Raphael ameishukuru serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suhulu Hassan kuwapa mkopo wa Tsh. Mil.10 inayotokana na fedha za 10% huku akiahidi kuzirejesha kabla ya mkataba wao wa miaka 2 kumalizika.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.