• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANUFAIKA WA TASAF MAGOMENI WASHUHUDIA WALIVYOONDOKANA NA UMASKINI , WAISHUKURU SERIKALI

Posted on: January 27th, 2025

Wananchi wa Kijiji cha Rose kata ya Magomeni Wilayani Kilosa wameeleza kuhusu mafanikio walioyapata kupitia mradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF) ambapo wamebainisha kuwa mfuko huo umewatoa kutoka katika hali duni ya umaskini wa kupindukia hadi kufikia hali ya wastani wa kuweza kupata mahitaji muhimu ya siku yakiwemo chakula, malazi na mavazi.

Wananchi hao wamesema hayo Januari 27, Mwaka huu wakati wa ziara ya viongozi wa TASAF kutoka Makao Makuu wakiongozwa na Mkurugenzi wa Miradi ya TASAF hapa nchini Bw. John Steven walipofanya ziara katika Kijiji cha Rose Kata ya Magomeni Wilayani Kilosa kwa lengo la kukagua miradi ya TASAF iliyotekelezwa Wilayani humo.

Wakielezea mafanikio hayo, wananchi wa Kijiji cha Rose Kata ya Magomeni akiwemo Bi. Dorothea Mbombwe amesema baada ya kubahatika kuwa mnufaika wa TASAF, fedha alizozipata zimemsaidia katika masomo na kuhitimu elimu ya Stashahada ya maendeleo ya jamii na kuiomba serikali kuendelea kusaidia kaya zinazokidhi vigezo ili nao waweze kuondokana na umaskini wa kupindukia.

"...kwenye suala la TASAF napenda kuishukuru kwa sababu imenisaidia kwenye suala zima la elimu mpaka hapa nilipofikia ngazi ya stashahada ya elimu ya maendeleo ya jamiii..." amesema Bi. Dorothea

Naye, Bi. Lilian Samwel kutoka kata hiyo ameishukuru Serikali kwa kuanzisha Mradi wa TASAF kwani amesema Mfuko huo umemsaidia kununua chereheni kinachomsaidia kujipatia kipato kwa ajili ya kuendesha familia yake ya kila siku.

Mkurugenzi wa Miradi ya TASAF Taifa Bw. John Steven amesema, TASAF imeweza kufanikisha miradi mingi ndani ya Mkoa wa Morogoro yenye thamani ya sh. Bil. 66, kati ya hizo zimetolewa kwa njia ya mtandao wa simu na kupitia benki, huku akieleza uwepo wa ajira za muda zikizotolewa ambapo zimetumia kiasi cha Tsh. Bil. 23 na kutekeleza miradi 1500 Mkoani humo .

Bw. John amebainisha mafanikio mengine makubwa yaliyofanyika Mkoani humo kuwa ni pamoja na kuwafikia walengwa 43000 kati yao 21000 wamehitimu katika mpango wa TASAF na kuunda vikundi zaidi ya 3000 vikiwa na wanachama zaidi ya 36000 katika hivyo vikundi vimeweza kupatiwa kiasi cha Ths. Mil. 522 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za vikundi vyao.

Kwa upande wake, Mratibu wa TASAF Mkoa wa Morogoro Bw. Jacob Kayange amesema moja ya masharti kwa walengwa wenye watoto wenye umri chini ya miaka mitano ni kuhudhuria kliniki kwa kupitia mpango wa ruzuku wa TASAF, hivyo amesema Mkoa huo umefanikiwa kwa 98% ya watoto walengwa kupelekwa kliniki na 89.3 % kwenda shule za msingi na sekondari na kwa sababu hiyo mpango wa TASAF umefanikisha watoto wa kaya masikini kwenda shule na kliniki.

Timu hiyo ya viongozi wa TASAF kutoka Makao makuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Miradi ya TASAF hapa nchini, leo imetembelea mradi wa mfereji wa maji wenye kingo za kuzuia mafuriko kwa makazi ya kijiji cha Rose, vikundi vya wanachama mbalimbali ambao ni wanufaika wa TASAF ambapo Wilayani humo ina walengwa 8,900 kati ya hao wanachama 2000 wameweza kuhitimu katika mpango huo.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.