• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waratibu Watakiwa Kuhakikisha Ushiriki wa Wananchi kwenye Miradi

Posted on: April 4th, 2025

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’i Issa, amewasisitiza waratibu wa uwezeshaji wananchi kiuchumi wa Wizara na Mikoa kuhakikisha wananchi wanawezeshwa katika shughuli mbalimbali za maendeleo zinazoinufaisha jamii.


Katibu Mtendaji huyo amesisitiza hayo wakati akifungua kikao cha NEEC na Waratibu wa Uwezeshaji ngazi ya Wizara na Mikoa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Edema iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, kikiwa na lengo la kukumbushana majukumu mbalimbali ya kazi na mafunzo kwa waratibu wapya.


Akifafanua zaidi, Bi. Beng’i Issa amesema wananchi wanapaswa kuhusishwa katika shughuli za kiuchumi za Taasisi, Wizara na Mikoa ili kuwawezesha kuwa na umiliki wa miradi hiyo, ikiwemo ya ujenzi, mikopo na mafunzo mbalimbali ya kuwaongezea ujuzi kwa ajili ya manufaa yao.


"...kazi kubwa wanayotakiwa kufanya waratibu katika maeneo yao ni kuhakikisha uwezeshaji wa wananchi unajitokeza katika shughuli za Wizara, Taasisi na Mikoa..." Amesema Katibu Mtendaji huyo.


Sambamba na hayo, Bi. Beng’i amesema Serikali ina program ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) inayolenga kuboresha utoaji wa mikopo ya 10% katika Halmashauri, uboreshaji wa uwezo wa kuingia katika manunuzi ya umma 30%, pamoja na kuangalia vipaumbele vya Mkoa husika na ushiriki wa wananchi katika shughuli mbalimbali zilizopo katika jamii.


Kwa upande wake, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Mkoani Morogoro, Dkt. Rozalia Rwegasira, ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi wa Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mkoani humo, amesema katika Mkoa huo kuna shughuli mbalimbali zinazofanyika hususan kilimo, biashara na ujenzi wa miradi ya maendeleo, ambapo hutoa kipaumbele kwa wazawa ili kukuza uchumi wao na wa Mkoa kwa ujumla.


Naye, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Mkoani Kilimanjaro, Bw. James Bwanali, amesema kupitia kikao hicho cha kujengeana uzoefu, hasa mafanikio waliyoyapata Mkoa wa Morogoro katika kuimarisha uchumi wa wananchi wengi kupitia program ya IMASA, ili kwenda kuitekeleza katika Mikoa yao.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.