• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WASEMAVYO WADAU WA MFUMO MPYA WA MANUNUZI - NeST.

Posted on: September 2nd, 2023

Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo ya mfumo mpya wa - NeST Bw. Leopold Ngirwa akitoa mafunzo kwa washiriki wa mafunzo hayo.

NeST, ni Mfumo mpya wa kielektroniki wa manunuzi ya Umma yaani National - e - Procurement System, mfumo ambao umeundwa na wazawa hapa nchini. Mfumo huo unaotarajiwa kuwa mbadala wa mfumo wa awali wa manunuzi ya Umma uliojulikana kama Tanzania National e Procurement System yaani TANePS.

Mwishoni Julai 31 hadi Agosti 4 mwaka huu, Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa ununuzi wa Umma – PPRA, ilianza rasmi kutoa mafunzo ya kwa wataalamu ngazi ya mikoa namna ya kutumia mfumo wa NeST, wataalamu sita kwa kila Mkoa wa Tanzania Bara.

Wataalamu hao walikuwa na jukumu la kuujua vema mfumo huo na kisha kwenda kufundisha Maafisaengine ndani ya mikoa yaani Halmashauri zote zilizopo katika Mkoa husika.

Mkoani Morogoro tayari Timu hiyo ya Wataalamu sita kutoka Sekretarieti ya Mkoa huo imekwisha tekeleza jukumu lake la msingi kwa kutoa mafunzo ya mfumo wa NeST kwa wataalamu 62 waliotoka Halmashauri zote tisa za Mkoa huo.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mbaraka Mwinshehe Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kufunguliwa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Utumishi Bw. Herman Tesha Kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa yalianza Agosti 28 yamehitimishwa Septemba Mosi huku akisisitiza washiriki kwenda kuwa wakufunzi kwa wengine mara warejeapo katika Halmashauri zao.

Washiriki nao waliusifu mfumo huo na kwamba una tija kubwa kwa watanzania;

Kwanza, wakitoa pongezi kwa Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada zake za kuwaendeleza watanzania na kuwaamini kuunda mfumo wa NeST.

Pili, kwa kuwa mfumo huo wa NeST umeundwa na wazawa wenyewe kuna uhakika wa asilimia kubwa mfumo utaongeza usiri na usalama kwa nyaraka za Serikali ukilinganisha na mfumo wa TANeMPS uliokuwa chini ya wageni.

Tatu, mfumo huu pia umeelezwa kuwa ni mfumo wa wazi kwa kuwa kila mchakato wa manunuzi ya Umma utakaofanyika ndani ya mfumo, kila aliyepewa dhamana ya kuingia kwenye mfumo huo atakuwa anaona au kujua kinachoendelea humo hivyo kupunguza changamoto ya rushwa wakati wa mchakato wa kutangaza zabuni.

Nne, mfumo huu utapunguza gharama kubwa ikiwemo matumizi  ya karatasi (Paper Works) Kwa kuwa mchakato wa ununuzi wa umma na utangazaji wa zabuni kwa kiasi kikubwa utatumika ndani ya mfumo.

Mkaguzi wa Ndani wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Steven Benedict akitoa mafunzo kwa washiriki wa mafunzo hayo ya mfumo mpya wa Manunuzi - NeST.

Akifunga mafunzo hayo, kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA katika Ofisi hiyo Bw. Herman Njelekela amewataka washiriki kwenda kuanza mara moja kuwafundisha wataalamu wengine kwa kuwa mfumo wa TANeMPS utazimwa ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu na Mfumo wa NeST kuunza kutumika.

Afisa Tehama kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Herman Njelekela akizungumza na washiriki wa mafunzo ya mfumo mpya wa NeST wakati wa kufunga mafunzo hayo.

Washiriki wa mfumo wa NeST nao walipata fursa na kuishukuru Serikali kwa kuleta mfumo huo na kwamba utaleta  chachu katika utendaji kazi wa Serikali na kurahisisha  shughuli za ununuzi hivyo kuharakisha kuleta maendeleo ya wananchi hususan katika ujenzi wa miradi ya maendeleo.

Pamoja na kutoa pongezi hizo kwa Serikali juu ya mfumo mpya wa NeST, walikuwa na maoni kwa serikali:

Bw. Hosam Issale (Mhasibu) Halmashauri ya Ulanga anasema ili mfumo wa NeST ufanye kazi ipasavyo viongozi wanaotakiwa kuingia kwenye mfumo huo wawe wepesi kukasim mamlaka yao kwa waliochini yao wanapokuwa hawana nafasi, hii itasaidia kuondoa ucheleweshaji wa mchakato ndani ya mfumo huo, vinginevyo mfumo huo utakuwa hauna manufaa kama inavyo tazamiwa na changamoto ya manunuzi kuchukua muda mrefu itabakia palepale.

Lakini pia Bw. Issale anasema mfumo huu Pamoja na uzuri wake wa kuwa mfumo wa wazi na unaotekelezeka haraka lakini unategemea sana mtandao, hivyo anaishauri Serikali kuimarisha zaidi Mtandao mahali mfumo ulipo lakini pia katika halmashauri husika.

Naye Bw. Nkwabi Simon (Mhandisi) Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi ameusifu mfumo wa NeST kuwa unapunguza gharama.

Aidha, Mhandisi Nkwabi maoni yake kwa PPRA ni kuhakikisha mfumo wa NeST unatumika kwenye matumizi ya fedha zinazopitia force Account ili kuokoa fedha nyingi za Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia Forse Account.

Serikali imeshatoa maelekezo kuwa mfumo wa TANePS utazimwa ifikapo mwezi Septemba mwaka huu na mfumo wa NeST utaanza kutumika rasmi kuanzia mwezi Oktoba mwaka huu, huku ikiwataahadharisha Wakuu wa taasisi kutofanya manunuzi yoyote ya umma nje ya mfumo wa NeST na watakaokwenda kinyume cha maagizo hayo watachululiwa hatua kali za kinidhamu.

Baadhi ya Washiriki wa mafunzo ya mfumo mpya wa Manunuzi - NeST wakielezea uelewa wao kuhusu mfumo huo baada ya kupatiwa mafunzo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.