• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

watakiwa kuachana na Imani potofu wakati wa Sensa.

Posted on: September 1st, 2021


Wananchi wa Mtaa wa Mtawala Kata ya Mwembesongo Mkoani Morogoro wametakiwa kuacha mila potofu dhidi ya jaribio la Sensa ya watu na makazi linalotarajiwa  kufanyika Septemba 11 mwaka huu.

Rai hiyo imetolewa na Kamishna wa Sensa Kitaifa Bi. Anne Makinda Septemba Mosi mwaka huu alipokuwa anazungumza na wananchi wa kata hiyo kwa lengo la kuwafahamisha umuhimu unaotokana na zoezi la Sensa ya watu na makazi.


Bi. Anne amebainisha kuwa, watu wengi wamekuwa na imani potofu juu ya zoezi la Sensa ya watu na makazi hali ambayo hupelekea baadhi yao kujiweka mbali na zoezi hilo kila inapotokea kufanyika.

‘’Hatufanyi Sensa kwa ajili ya Siasa, chama wala kwa dini yoyote isipokuwa ni kwa ajili ya maendeleo ya watanzania’’ amesema Makinda.

Aidha, Makinda amewataka wananchi hao kutoa ushirikiano kwa viongozi watakaokuja kuhesabu kaya zao na kusaidia kujibu maswali ambayo yameorodheshwa katika madodoso ya Sensa.

Sambamba na hayo, Makinda amesema iwapo zoezi la Sensa na makazi litafanyika vizuri litaisaidia Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kutambua matumizi bora ya kodi zinazotolewa na wananchi.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema Mkoa wa Morogoro umejipanga vizuri katika zoezi zima la Sensa ya watu na makazi na tayari wameshafanya uteuzi wa kamati kwa ajili ya zoezi hilo.

Licha ya uteuzi wa kamati hizo, Shigela ameeleza kuwa hadi sasa kamati hiyo imeshatambua idadi ya kaya kwenye vijiji, vitongoji na mitaa yote ili kurahisisha zoezi la kuhesabu watu muda utakapofika.

‘’…Lakini pia tumeweza kuwa na namba za mawasiliano za viongozi wa maeneo hayo. kiongozi wa Mtaa, Kijiji na Kitongoji ili kurahisisha  shughuli za Sensa akiwa amepangiwa kitongoji fulani hatuhangaiki kutafuta mawasiliano yao’’ amesema Shigela.

Naye, Katibu Tawala Msaidizi kwa upande wa Mipango na Uratibu Anza Amen Ndossa ambaye pia ni Mratibu wa Sensa Mkoa wa Morogoro amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika kushiriki zoezi hilo kwa lengo la kuwa na Sensa itakayoleta ufanisi na matokeo chanya kwa Taifa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.