• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WATENDAJI SERIKALINI WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU KATIKA KUWATUMIKIA WANANCHI.

Posted on: February 6th, 2023

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amewataka watendaji wa Serikali kuwajibika katika nafasi zao wanazozitumikai kwa kusikiliza na kutatua changamoto  za wananchi na huku akiwatahadharisha kuwa serikali ya awamu ya sita haitomfumbia macho mtendaji yeyote ambaye hatoendana na kasi ya serikali iliyopo madarakani.

Daniel Chongolo amesema hayo Februari 5 mwaka huu kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 46 ya kuzaliwa kwa chama hicho yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kiwanja cha Ndege katika Manispaa ya Morogoro.

Katibu Mkuu huyo amesema, haiwezekani Serikali itoe fedha kwa ajili ya kutatua changamoto za wananchi halafu wale wenye dhamana ya kutatua changamoto hizo hawatimizi wajibu wao.

“...tunachotaka kuona ni kila kilicho ahidiwa na kikatolewa fedha na Serikali, fedha ile inaenda kuleta matokeo ya kubadilisha maisha ya mwananchi na sio maneno na hadithi..” amesema Daniel Chongolo.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb) amesema Serikali ya awamu ya sita imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa inapunguza mfumuko wa bei hapa nchini.

Waziri Bashe amesema ili kufikia hatua hiyo serikali ni kuanza  kununua mazao kutoka kwa wakulima na kuyahifadhi katika maghara ya Serikali ambapo mpaka sasa tayari wamehifadhi tani 23 za mahindi, na kwamba Serikali itawauzia wananchi wake kwa bei ya shilingi 700 kwa kilo.

Aidha, ameogeza kuwa Serikali imetoa tani 247,000 za mbolea za ruzuku kwa ajili ya kuleta tija kwenye kilimo na kuongeza uzalishaji.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa wakati akitoa salamu za Mkoa ameishukuru Serikali ya CCM kwa kutekeleza kwa vitendo ilani ya chama hicho kwa kuwaondolea kero mbalimbali wanamorogoro ikiwemo kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama maji, barabara, umeme pamoja na kutatua migogoro ya ardhi na ile ya wakulima na wafugaji.

Maadhimisho hayo ya kuzaliwa kwa CCM yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo, Katibu wa Itikadi na Uenezi Bi. Sofia Mjema, Katibu wa Organization na Siasa, mawaziri na Manaibu Mawaziri wa Sekta  za Maji, Ardhi, Mifugo na Uvuvi, Tamisemi na Kilimo, Wabunge wa Mkoa wa Morogoro, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na wananchi.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.