• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WATOTO ZAIDI YA 400, 000 KUCHANJWA POLIO MKOANI MOROGORO.

Posted on: May 19th, 2022

Watoto 423,000 walio chini ya Miaka mitano wanatarajiwa kupata chanjo ya Polio Mkoani Morogoro ili kuwakinga na ugonjwa huo, hii ni baada ya kupatikana kwa taarifa za kuwepo kwa ugonjwa huo katika nchi jirani ya Malawi.




Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Mei 18 mwaka huu wakati akizindua chanjo ya Polio kwa Watoto walio na umri chini ya miaka mitano Mkoani humo, zoezi ambalo limefanyika katika Viwanja vya Kituo cha Afya cha Sabasaba Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Uzinduzi huo umefanyika ikiwa ni ishara ya jitihada za Serikali za kuwalinda Watoto wa umri huo hapa nchini ili wasipate maambukizi na mashambulizi hatari ya Ugonjwa wa Polio.






Akiongea na hadhara iliyokuwepo katika viwanja hivyo, Martine Shigela amewataka Wazazi Mkoani humo kuhakikisha Watoto wao wanapata chanjo hiyo kwani Serikali imejipanga vema kupitia Watendaji wa ngazi zote kuhakikisha wanapita kila Kaya yenye Watoto walio chini ya Miaka mitano wanapatiwa chanjo hiyo.

“Mkoa wetu umejipanga kuchanja zaidi ya watu 423,000 na Wataalamu wetu wamejipanga vizuri kuhakikisha kila Familia yenye Mtoto ‘under five’ chini ya Uongozi wa watendaji wetu wa Mitaa, vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji na Wenyeviti wa Vijiji wanatembela Familia hizo na watoto hao wanapatiwa chanjo ya matone...” amesema Shigela.




Katika hatua nyingine Martine Shigela amebainisha kuwa mara ya mwisho Ugonjwa huo ulibainika nchini Tanzania Mwaka 1996, hivyo, kufanyika kwa uzinduzi wa chanjo hiyo leo, haina maana kwamba ugonjwa huo umeingia nchini kwetu la hasha, bali Serikali imefikia hatua hiyo ili kuchukua tahadhari baada ya taarifa za uwepo ugonjwa huo katika nchi jirani ya Malawi.






Kwa upande wake Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Paschal Kihanga amewapongeza wazazi wa Watoto wanaoishi katika Manispaa hiyo kwa hamasa walioionesha ya kuwapeleka watoto kupata chanjo ya Polio katika kituo hicho cha Afya.





Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio ameweka wazi kuwa Ugonjwa wa Polio hauna dawa na mara nyingi huwaathiri watoto wa umri huo na kupelekea ulemavu wa kudumu kwa mtoto na kwamba huambukiza kama yanavyoambukiza magonjwa mengine ya kuhara, hivyo amewataka wanajamii wajitokeze kwa wingi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo kwani chanjo hiyo ni salama.




Kwa upande wake mwakilishi wa Taasisi ya Centers for Diseases Control and Prevention (CDC) Bw. Philip Talboy amesema kuwa Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Serikali pamoja na wanajamii wenyewe kwa kushirikiana pamoja, kutawezesha kukomesha na kuondoa na kuuondoa Ugonjwa wa Polio ndani ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.






MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.