• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WATOTO ZAIDI YA 400, 000 KUCHANJWA POLIO MKOANI MOROGORO.

Posted on: May 19th, 2022

Watoto 423,000 walio chini ya Miaka mitano wanatarajiwa kupata chanjo ya Polio Mkoani Morogoro ili kuwakinga na ugonjwa huo, hii ni baada ya kupatikana kwa taarifa za kuwepo kwa ugonjwa huo katika nchi jirani ya Malawi.




Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Mei 18 mwaka huu wakati akizindua chanjo ya Polio kwa Watoto walio na umri chini ya miaka mitano Mkoani humo, zoezi ambalo limefanyika katika Viwanja vya Kituo cha Afya cha Sabasaba Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Uzinduzi huo umefanyika ikiwa ni ishara ya jitihada za Serikali za kuwalinda Watoto wa umri huo hapa nchini ili wasipate maambukizi na mashambulizi hatari ya Ugonjwa wa Polio.






Akiongea na hadhara iliyokuwepo katika viwanja hivyo, Martine Shigela amewataka Wazazi Mkoani humo kuhakikisha Watoto wao wanapata chanjo hiyo kwani Serikali imejipanga vema kupitia Watendaji wa ngazi zote kuhakikisha wanapita kila Kaya yenye Watoto walio chini ya Miaka mitano wanapatiwa chanjo hiyo.

“Mkoa wetu umejipanga kuchanja zaidi ya watu 423,000 na Wataalamu wetu wamejipanga vizuri kuhakikisha kila Familia yenye Mtoto ‘under five’ chini ya Uongozi wa watendaji wetu wa Mitaa, vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji na Wenyeviti wa Vijiji wanatembela Familia hizo na watoto hao wanapatiwa chanjo ya matone...” amesema Shigela.




Katika hatua nyingine Martine Shigela amebainisha kuwa mara ya mwisho Ugonjwa huo ulibainika nchini Tanzania Mwaka 1996, hivyo, kufanyika kwa uzinduzi wa chanjo hiyo leo, haina maana kwamba ugonjwa huo umeingia nchini kwetu la hasha, bali Serikali imefikia hatua hiyo ili kuchukua tahadhari baada ya taarifa za uwepo ugonjwa huo katika nchi jirani ya Malawi.






Kwa upande wake Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Paschal Kihanga amewapongeza wazazi wa Watoto wanaoishi katika Manispaa hiyo kwa hamasa walioionesha ya kuwapeleka watoto kupata chanjo ya Polio katika kituo hicho cha Afya.





Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio ameweka wazi kuwa Ugonjwa wa Polio hauna dawa na mara nyingi huwaathiri watoto wa umri huo na kupelekea ulemavu wa kudumu kwa mtoto na kwamba huambukiza kama yanavyoambukiza magonjwa mengine ya kuhara, hivyo amewataka wanajamii wajitokeze kwa wingi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo kwani chanjo hiyo ni salama.




Kwa upande wake mwakilishi wa Taasisi ya Centers for Diseases Control and Prevention (CDC) Bw. Philip Talboy amesema kuwa Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Serikali pamoja na wanajamii wenyewe kwa kushirikiana pamoja, kutawezesha kukomesha na kuondoa na kuuondoa Ugonjwa wa Polio ndani ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.






MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA NANENANE YASHIKA KASI MOROGORO

    June 29, 2022
  • Kamati ya Bunge yashauri wananchi Wilayani Mvomero kukubali kutumia mbinu kukabiliana na wanyama wakali

    June 27, 2022
  • RC MOROGORO APONGEZA UTENGENEZAJI MADAWATI 400 DUTHUMI.

    June 26, 2022
  • RC aendelea na ziara Wilaya ya Morogoro, atatua migogoro ya wananchi.

    June 24, 2022
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.