• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI BASHE APIGA MARUFUKU UKODISHAJI MASHAMBA WANANCHI.

Posted on: February 4th, 2023

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe (Mb) amepiga marufuku ukodishaji wa mashamba kwa wananchi wa Wilaya ya Kilosa huku akiagiza uongozi wa Halmashauri na Wilaya hiyo kuacha kuwakodishia mashamba wananchi badala yake waweke utaratibu wa kuwagawia mashamba hayo Kwa mfumo wa ‘block farms’ ili wananchi hao waweze kukuza uchumi wao.


Waziri Bashe ametoa agizo hilo Februari 4 mwaka huu wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mvumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua skimu za umwagiliaji pamoja na kusikiliza kero za wakulima.

Aidha, ziara ya Bashe ni utekelezaji wa agizo la Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo alilolitoa hivi karibuni wakati wa ziara yake Wilayani humo, likimtaka Waziri huyo kufanya ziara katika Mkoa huo hususan wilaya ya Kilosa.

Waziri Bashe amesema Serikali kupitia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefuta mashamba 67 yenye jumla ya ekari 2700 ambayo yalikuwa hayaendelezwi na wawekezaji na kuagiza mashamba hayo kugawanywa Kwa wananchi wa maeneo hayo.

Aidha, amesema Halmashauri hiyo imekuwa ikiwatoza wananchi shilingi 10,000 Kama Kodi ya mashamba na kupiga marufuku mfumo huo na kuwataka kuacha kupokea fedha hizo kutoka Kwa wananchi badala yake watumie mfumo wa Block farms.

".. ni marufuku Halmashauri kuwakodisha mashamba wananchi..wakulima wasikodishiwe mashamba yaliyofutwa hati na Rais Samia Suluhu Hassani...” Amesema Waziri Bashe.

Sambamba na hilo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilosa Bwana Kisena Mabuba Kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na wataalamu wa ardhi kuyapima mashamba hayo na kuyagawa Kwa wananchi Kwa mfumo wa ‘block farms’ Kwa lengo la kuyaendeleza.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo wa kilimo amekiagiza Chama Cha Ushirika cha UWAWAKUDA cha Dakawa Wilayani Mvomero kulipa fedha kiasi cha shilingi milioni 62 kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Umwagiliaji ifikapo Februari 6 na kuwasilisha  nakala za makusanyo ya Mfuko wa Maendeleo ya Ushirika kwa Mkuu wa Mkoa huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa wakati akitoa shukrani kwa ujio wa Waziri huyo amemuomba kupatiwa wakaguzi kwa lengo la kufanya uchunguzi wa kina katika chama cha ushirika wa UWAWAKUDA ili kubaini viashiria vya ubadhirifu wa fedha za wakulima na wanachama wa Ushirika huo.

Akielezea changamoto zinazoikumba Skimu ya Wami – Luindo Bi. Maimuna Makukika  Mhandisi umwagiliaji Wilaya ya Mvomero amesema Skimu hiyo ina mifereji michache ambayo inakidhi hekta 172 tu huku skimu hiyo ikiwa na jumla ya hekta 956, za umwagiliaji, hivyo wakulima wameomba kujengewa mifereji mingine ili kuongeza ufanisi katika kilimo hicho.

Aidha, ameongeza kuwa mafuliko hasa katika kipindi hiki cha mvua nyingi unaathiri uzalishaji wao kutokana na mashamba yao kujaa maji yanayotokana na mafuliko.

Waziri Bashe wakati wa ziara yake ametembelea Skimu za umwagiliaji za Wami – Luindo, mashamba ya chama cha Ushirika cha UWAWAKUDA, na Skimu ya Rudewa iliyopo Wilayani Kilosa na kufanya mikutano ya hadhara kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi wa maeneo hayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.